Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na kukuza usawa wa kijinsia na kuwaezesha wanawake, UN Women limehitimisha mkutano wake wa mwaka mwishoni mwa wiki hii mjini New York Marekani kwa makubaliano kuhusu njia za kulinda na kuboresha jinsi wasichana na wanawake watakavyoweza kufikia mifumo ya ulinzi wa kijamii, huduma za kijamii na miundombinu endelevu.
Ikiwa leo ni siku ya maji duniani, maudhui yakiwa hakuna kumwacha mtu nyuma katika kupata huduma hiyo ifikapo mwaka 2030 kwa kuzingatia lengo namba 6 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, Tanzania imetaja hatua iliyochukua ili kufanikisha lengo hilo.
Mkutano wa 63 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW, ukiwa umeingia siku ya pili kwenye mako makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, hii leo baadhi ya mada ambazo zimejadiliwa ni wanawake na uongozi.
Mkutano wa 63 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW unaanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ukileta pamoja zaidi ya washiriki 9000 kutoka wawakilishi wa nchi 193 wanachama wa umoja huo pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa na yale ya kiraia.