Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

CRC

Watoto wakimbizi kutoka Somalia wakiwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya ambako WFP inawapatia misaada ya dharura.
WFP/Rose Ogola

Majanga yanavyozidi kushamiri isiwe kisingizio cha kusigina haki za mtoto- UN

Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa hususan zile za mtoto wametoa taarifa ya pamoja hii leo huko Geneva, Uswisi wakisema  majanga ya kiafya, kibinadamu na yale  yanayohusiana na tabianchi yakizidi kuongeza changamoto kubwa duniani kila uchao kama vile ukimbizi wa ndani, ukatili wa kingono na njaa, serikali lazima zikumbuke kuwa watoto wana haki kamilifu za kimsingi za kibinadamu na kwamba haki hizo zinapaswa kulindwa.

06 OKTOBA 2022

Hii leo katika Habari za UN Assumpta Massoi anakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Kujifunza Lugha ya Kiswahili.

Katika Habari kwa Ufupi kuna haki za mtoto kuzingatiwa hasa wakati huu ambapo majanga ya kiasili na yanayosababishwa na binadamu  yanakengeua utekelezaji wa haki za mtoto. Suala la afya ya akili barani Afrika ambayo inachochea matukio ya kujiua ,na WHO imezindua kampeni maalum. Na kisha ni uzinduzi wa ripoti kuhusu matumizi ya matukio makubwa ya michezo ili kuimarisha afya ya mwili ya binadamu.

Sauti
11'26"
© UNICEF/UN0346146/Diefaga

Jamii inasemaje kuhusu mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto?

Makala ya leo imejikita na mkataba wa haki za mtoto duniani uliopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa miaka 30 iliyopita ukisimamia nguzo kuu nne ambazo ni haki ya kutobaguliwa, kuhakikisha mahitaji yake yanatimizwa, haki ya kuishi na kuendelezwa na haki ya kusikilizwa. Na je tangu kupitishwa kwa mkataba huo, jamii, wazazi na watoto wenyewe wanauelewaje mkataba huo? Na una maana gani kwao? Ungana na Flora Nducha

 

Sauti
5'53"
UNICEF

Watoto wanasemaje kuhusu mkataba wa kimataifa wa haki za watoto?

Ikiwa leo ulimwengu unaadhimisha siku ya kimataifa ya mtoto,  makala ya Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa inajikita mkoani Morogoro nchini Tanzania ambako watoto wanatoa maoni yao kuhusu siku yao hii na pia mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto, CRC,  ambao umetimiza miaka 30 tangu ulipopitishwa.

Siku ya mtoto duniani ilianzishwa mwaka 1954 na huadhimishwa tarehe 20 mwezi Novemba ya kila mwaka ili kusongesha utangamano na ustawi wa kimataifa miongoni mwa watoto wote duniani.

Sauti
3'13"

18 NOVEMBA 2019

Miongoni mwa Habari anazokuletea Flora Nducha katika Jarida la Habari hii leo

-Miaka 30 ya mkataba wa Haki za mtoto duniani CRC, kuna mafanikio kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF  lakini pia changamoto zinaendelea kwa watoto masikini

-Muungano wa Afrika AU na shirika la afya duniani WHO waanzisha ubia mpya ili kushirilkiana katika kutimiza malengo ya afya 

-Wakimbizi Sudan Kusini wasema wameambiwa amani imerejea Yambio sasa wanaanza kurejea nyumbani je nini wanakikuta huko?

Sauti
11'18"