Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema ingawa ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, unakwamisha harakati za kufuatialia visa vya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto katika kambi ya wakimbizi warohingya huko Bangladesh, bado kuna mbinu zinatumika kupatia msaada manusura.