Chuja:

Costa Rica

OHCHR Regional Office for Centra

Catalina:Tunataka watambue kuwa kuna binadamu wanaojali binadamu wenzao

Catalina, si jina lake halisi, ni mwanasheria kutoka Nicaragua mwenye umri wa miaka 44 na ambaye alikimbilia nchi jirani ya Costa Rica ili kunusuru maisha yake na ya watoto wake wawili. Flora Nducha na maelezo zaidi.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linasema kuwa Catalina hivi sasa ni mkimbizi Costa Rica. 

Mwaka 2018 wakati wa maandamano dhidi ya serikali nchini Nicaragua, Catalina alifungua milango ya nyumba yake ili kusaidia waandamanaji ambapo aliwapatia chakula pamoja na huduma ya kwanza pindi walipopata majeruhi. 

Sauti
2'21"
Wanicaragua wakiwa wanasubiri kufanya maombi ya hifadhi katika ofisi ya uhamiaji katika mji mkuu wa Costa Rica, San Jose (Agosti 2018)
UNHCR/Roberto Carlos Sanchez

Mwaka mmoja wa mgogoro wa Nicaragua, zaidi ya watu 60,000 wameikimbia nchi.

Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbiazi UNHCR Liz Throssell amewaambia wana habari hii lemjini Geneva Uswisi kuwa inakadiriwa kuwa watu wapatao 62,000 wameikimbia Nicaragua na kusaka hifadhi katika nchi za jirani wengi wao kufikia 55,500 wakiingia Costa Rica kutokana na mazingira magumu nchini mwao tangu mwaka jana.

 

Kutoka kulala mitaani hadi kumiliki duka la mikate Costa Rica

Nchini Costa Rica sera ya kuwezesha wakimbizi kufanya kazi imeleta nuru kwa raia wa Colombia waliokimbia machafuko nchini mwao. Flora Nducha na ripoti kamili.

(Taarifa ya Flora Nducha)

Miaka 17 iliyopita, ghasia nchini Colombia zilisababisha Miriam Velásquez na mumewe Ricardo Ángel kukimbia nchi yao na kusaka hifadhi nchini Costa Rica.

Baada ya kuwasili kwenye mji mkuu San Jose, familia hiyo haikuwa na kipato chochote na hivyo kujikuta wanaishi mitaani.