Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

COP24

UN News/Yasmina Guerda

Viongozi wakifahamu kuhusu mabadiliko ya tabianchi, kazi inakuwa rahisi: UNEP

Mkutano wa 24 wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi (COP24) umekamilika huko mjini Katowice Poland. Baada ya wiki mbili za majadiliano ya makundi zaidi ya 200 yameidhinisha muongozo wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mwaka 2015, wenye lengo lakupunugza ongezeko la joto duniani kuwa chini ya nyuzi joto 2.

Mkutano huo umeeleza kuwa ingawa kuna hatua ambazo zimepigwa, lakini bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kufikia makubaliano ya mkataba wa Paris hasa kwa nchi zinazoendelea.

Sauti
2'41"
Kikao chamwisho cha mkutano wa COP24 Katowice, Poland,16 Disemba 2018.
UNFCCC/James Dowson

Baada ya vuta ni kuvute ya wiki mbili muafaka wafikiwa COP24

Baada ya wiki mbili za majadiliano ya makundi zaidi ya 200 yaliyokusanyika Katowice, Poland kwa ajili mkutano wa Umoja wa  Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi , COP24 ,yameidhinisha  muongozo wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mwaka 2015, wenye lengo la kupunguza ongezeko ka joto duniani kuwa nchini ya nyuzi joto 2 ikilinganishwa na viwango vya kabla ya wakati wa viwanda.

Katibu Mkuu wa UN António Guterres alipokuwa akizungumza hii leo tarehe 12 Desemba 2018 na wajumbe wanaoshiriki COP24 huko Katowice Poland
UNFCCC Secretariat/James Dowson

Guterres afananisha kutotimiza mkataba wa mabadiliko ya tabianchi na kujiua

Wakati ambapo majadiliano kuelekea mpango madhubuti wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi wa mwaka 2015 yakiendelea kukumbwa na vikwazo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo hii amerejea Katowice, Poland kuwapa changamoto zaidi ya viongozi 100 wa serikali ambao wanakutana katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabia nchi COP24 kufikia makubaliano na kuikamilisha kazi.

Kimbunga Hagupit kilipopiga Ufilipino tarehe 5-6 Desemba 2014, hali ilikuwa mbaya kwani nchi  hiyo bado ilikuwa haijasahau madhara ya kimbunga Haiyan kilichotokea Novemba 2013.
OCHA/Jennifer Bose

Mamia wakielekea Marrakech, CO24 nayo yajadili tabianchi na uhamiaji

Wakati mamia ya watunga sera wakikusanyika huko Marrakech nchini Morocco kwa ajili ya kukubaliana juu ya mkataba mpya wa kimataifa kuhusu uhamiaji, mkutano wa 24 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP24 huko Katowice Poland, nao unajikita katika njia thabiti za kusaidia nchi kukabiliana na ukimbizi wa ndani  utokanao na madhara ya mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ukosefu wa maji, mafuriko, vimbunga na kuongezeka kwa kina cha maji ya bahari