Ban akaribisha tamko la COP22:
[caption id="attachment_301713" align="alignleft" width="300"]bancop22
"Enzi mpya ya utekelezaji na hatua" kuhusu mabadiliko ya tabia nchi:COP22
Nchi zilizokusanyika kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabia au COP22 , zimetangaza tamko la “enzi mpya ya utekelezaji na hatua kuhusu mabadiliko ya tabia nchi.”Tamko la hatua la Marrakech, limetolewa leo Ijumaa siku ya mwisho ya mkutano huo uliokunja jamvi nchini Morocco, likisema, jumuiya ya kimataifa ina wajibu wa haraka wa kuchukua hatua dhidi ya dunia inayozidi kuchemka , ili kuhakikisha kiwango cha joto kinasalia chini ya nyuzi joto 2 celsius.
Afrika kufaidika kwanza na mfumo wa tahadhari ya majanga:COP22
Nchi za Afrika zenye maendeleo dunia na visiwa vya Pacific watakuwa wa kwanza kufaidika na mfumo ulioboreshwa wa tahadhari dhidi ya hali ya hewa na athari zinazohusiana na mabadiliko ya tabia nchi kupitia mkakati wa kuchukua hatua ulioainishwa na mkutano wa Umoja wa mataifa wa mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea Morocco.
Nchi hizo zikiwemo Mali, Burkina Faso, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC nan chi za visiwa vidogo zinazoendelea , zitapatiwa msaada wa awali wa dola milioni 12 zilizotengwa na mradi wa athari za mabadiliko ya tabia nchi na tahadhari ya mapema (CREWS).
COP22: Tanzania yaendelea kutekeleza miradi ya kuhimili tabianchi- Makamba
Tanzania imesema miradi ya kuhimili mabadiliko ya tabianchi inaendelea kutekelezwa nchini humo licha ya kusuasua kwa uchangiaji wa fedha kutoka nchi zinazoongoza kwa utoaji wa hewa chafuzi duniani.