Vita ya Ukraine imetuletea adha dunia nzima: Azali Assoumani
Rais wa kisiwa cha Comoro Azali Assoumani akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu kikao cha 77 amesema jumuiya ya kimataifa hivi sasa inakabiliwa na changamoto lukuki, kuanzia athari za kiafya kama janga la COVID-19 ambalo linaingia mwaka wa tatu ssasa, mabadiliko ya tabianchi hadi vita ya Ukraine ambayo imeleta adha kwa dunia nzima.