Serikali na upinzani wanaposhikamana hakuna linaloharibika
Azma ya serikali ya Colombia na kikundi cha FARC ya kuhakikisha wanatekeleza makubaliano ya amani, imekuwa ni chachu ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa.
Wakimbizi wa Venezuela huko Colombia wapitia madhila mengi
Raia wa Venezuela wanaokimbilia Colombia kusaka mlo na huduma za tiba wamesimulia madhila wanayokumbana nayo ikiwemo uhaba wa huduma hata huko wanakokimbilia.
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la mpango wa chakula duniani, WFP David Beasley amenukuu simulizi hizo akizungumza na waandishi wa habari huko Bogota, Colombia akisema kuwa kutokana na shida huko Venezuela, raia kati ya elfu 40 na elfu 50 wanavuka mpaka kila siku na kuingia eneo la Cúcuta nchini Colombia.
Akinukuu baadhi ya simulizi hizo Bwana Beasley amesema..
(Sauti ya David Beasley)
Colombia yahitaji msaada kusaidia wakimbizi kutoka Venezuela
Simulizi za watoto wa kike kulazimika kutumbukia kwenye biashara ya ngono ili waweze kujikimu maisha au watoto wa kiume kulazimika kuingia kwenye magenge haramu zimeshamiri miongoni mwa raia wa Venezuela wanaokimbilia Colombia.
Waasi Colombia washambulia bomba la mafuta
Nchini Colombia, mashambulio ya bomu yameripotiwa hii leo kwenye bomba la kusafirisha mafuta la Cano Limon katika majimbo ya Arauca na Boyaca, ikiwa ni siku moja tu baada ya kumalizika kwa muda wa makubaliano ya muda ya kusitisha mapigano kati ya serikali na kikundi cha National Liberation Army, ELN.
Kutoka kulala mitaani hadi kumiliki duka la mikate Costa Rica
Nchini Costa Rica sera ya kuwezesha wakimbizi kufanya kazi imeleta nuru kwa raia wa Colombia waliokimbia machafuko nchini mwao. Flora Nducha na ripoti kamili.
(Taarifa ya Flora Nducha)
Miaka 17 iliyopita, ghasia nchini Colombia zilisababisha Miriam Velásquez na mumewe Ricardo Ángel kukimbia nchi yao na kusaka hifadhi nchini Costa Rica.
Baada ya kuwasili kwenye mji mkuu San Jose, familia hiyo haikuwa na kipato chochote na hivyo kujikuta wanaishi mitaani.
Pagination
- First page
- Previous page
- …
- 2
- 3
- 4
- 5
- 6