Chuja:

colombia

Waliokuwa wapiganaji wa FARC wakiwa kwenye mazungumzo na viongozi wa kijami nchini Colombia kama njia ya kujumuishwa tena kwenye jamii.Htua hiyo imewezesha kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini humo
Jennifer Moreno/UN Verification Mission

Hatua ya wagombea urais Colombia ni ya kuigwa:Zeid

Kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa , Zeid Ra'ad Al Hussein amepongeza hatua ya wagombea kiti cha urais nchini Colombia ya kuapa kuheshimu , kulinda na kuhakikisha haki za binadamu endapo wakichaguliwa na kukiita ni kitendo cha  kuvutia na kisicho na kifani.

Usalama mpakani mwa Ecuador na Colombia vyatutia hofu- UN

Umoja wa Mataifa umeeleza wasiwasi wake juu ya kuendelea kuzorota kwa hali ya usalama mpakani mwa Ecuador na Colombia.

Kauli hiyo inafuatia kitendo cha hivi karibuni cha kutekwa nyara na hatimaye kuuawa kwa wafanyakazi watatu wa vyombo va habari huko Ecuador sambamba na kutekwa kwa raia wawili wengine wa Ecuador.

Yaripotiwa kuwa watu hao ambao ni waandishi wa habari wawili na dereva mmoja walitekwa nyara tarehe 26 mwezi uliopita na hatimaye kuthibitishwa kuwa wameuawa tarehe 13 mwezi huu kwenye eneo hilo la mpakani.

Sauti
1'15"
Picha:WFP

Misaada yafikia wakimbizi wa ndani kusini mwa Libya

Hatimaye misafara iliyosheheni misaada ya kibinadamu imewafikia wakimbizi wa ndani nchini Libya waliopo mji wa Marzuk kusini mwa nchi hiyo.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linasema wakimbizi hao ni manusura wa mapigano ya hivi karibuni kati ya vikundi vilivyojihami kwenye mji wa Sabha, ulioko takribani kilimeta 760, kusini mwa mji mkuu wa Libya, Tripoli.

Sauti
1'27"