Skip to main content

Chuja:

choo

Lucy Adjeley Boye, mmoja wa wanufaika wa mradi wa Benki ya Dunia wa ujenzi wa vyoo imara na salama kwenye mji mkuu wa Ghana, Accra
Video Benki ya Dunia

Kujisaidia kwenye vifuko vya nailoni kumebakia historia- Mkazi wa Accra

Nchini Ghana, huko Afrika Magharibi ukosefu wa choo umekuwa ni adha kubwa kwa wakazi wa kitongoji kimoja maarufu kwa utalii kwenye mji mkuu Accra. Vifuko vya nailoni vilivyosheheni haja kubwa vilikuwa ni jambo la kawaida hadi Benki ya Dunia ilipoingilia kati na kusaidia mamlaka ya majisafi na majitaka ya jiij la Accra, GAMA. Sasa kuna ahueni na wananchi wamefunguka macho.
 

29 Novemba 2021

Karibu kusikiliza jarida ambapo jumatatu ni siku ya mada kwa kina na leo tunabisha hodi nchini Ghana kumulika adha za kukosa choo na jinsi Benki ya Dunia imeleta ahueni kwa familia husika kwenye mji mkuu wa taifa hio la Afrika Magharibi, ACCRA.

Pia utapata fursa ya kusikiliza habari kwa ufupi zikimulika masharti yaliyowekwa na Afrika kwa wanaotaka kutoa chanjo, kikao maalum cha WHO baada ya kutokea aina mpya ya kirusi pamoja na ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN kwa siku ya mshikamano na watu wa palestina. 

Sauti
11'12"
Picha ya maktaba ya UM

Tulianzisha shirika la mazingira ili kupambana na uchafu na ukosefu wa ajira-Sam Dindi  

Ikiwa leo ni siku ya choo duniani, Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO, linaeleza kuwa Ulimwenguni, asilimia 80 ya maji taka yanayozalishwa na jamii yanarudi katika mzunguko wa ikolojia bila kusafishwa,  na vilevile taka mwili za binadamu zisizodhibitiwa mathalani kwa kuwekewa dawa za kuua vijidudu, huingia kwenye mazingira na kueneza magonjwa hatari na sugu.   

Sauti
4'31"

Huduma za vyoo Buyenzi nchini Burundi ni tatizo

Ukosefu wa huduma  safi ya vyoo   ni changamoto kubwa  sana katika nchi zinazoendelea kutokana na miundombinu mibovu  katika   nchi nyingi zinazoendelea kuanzia Afrika, Asia, Ulaya hadi Amerika. Umoja wa Maaifa unasema kuwa takribani asilimia 60 ya wakazi wa dunia hawana kabisa choo kwenye makazi yao. Kama hiyo haitoshi, watu milioni 862 wanajisaidia nje na hivyo kuhatarisha afya siyo tu za kwao bali pia za jamii nzima.

Sauti
3'49"

Choo chako ni salama?

Utafiti umebaini kwamba ukosefu wa vyoo safi  na salama ni hatarishi kwa afya ya binadamu. Takwimu za mashirika ya ufya ulimwenguni kama WHO na wengine zinaonyesha kuwa jamii zinazoishi katika mazingira yasiyo na vyoo salama zipo katika athari za kupatwa na milipuko ya magonjwa yatokanayo ya ukosefu wa matumizi salama ya vyoo kama kipindupindu na magonjwa mengine.