Mashirika ya Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na la mpango wa chakula duniani WFP yameonya kwamba ukata wa ufadhili, vita, majanga, changamoto za usambazaji misaada, ongezeko la bei ya vyakula na kupoteza kipato kutokana na janga la corona au COVID-19 vinatishia kuwaacha mamilioni ya wakimbizi barani Afrika bila chakula.