Jifunze Kiswahili- Shairi: Imekuwaje?
Hii leo kwenye Neno la Wiki tunasikiliza shairi kutoka kwake mwanariwaya na mwanachama wa Chama cha Kiswahili cha Kitaifa nchini Kenya, CHAKITA, Ken Walibora akighani shairi lake, Imekuwaje? Karibu!
Hii leo kwenye Neno la Wiki tunasikiliza shairi kutoka kwake mwanariwaya na mwanachama wa Chama cha Kiswahili cha Kitaifa nchini Kenya, CHAKITA, Ken Walibora akighani shairi lake, Imekuwaje? Karibu!
Na leo katika neno la wiki inaelezewa sentensi ambayo imejadiliwa sana kwenye mitandao ya kijamii na kwingine isemayo, baba alimpiga binti yake kwa kuwa alilewa.
Mchambuzi wetu Ken Walibora, mwanariwaya na mwanachama wa Chama Cha Kiswahili cha Kitaifa nchini Kenya, CHAKITA anaelezea sentensi baba alimpiga binti yake kwa kuwa alilewa.
Katika Neno la Wiki hii leo tunachambua methali isemayo, "Ukikaa na Simba, vaa ngozi ya mamba." Mchambuzi wetu ni Ken Walibora, mwanariwaya na na mwanachama wa Chama Cha Kiswahili cha Kitaifa nchini Kenya, CHAKITA. Fuatana naye mlumbi huyu wa lugha ya Kiswahili.
Katika Neno la wiki hii Mchambuzi wetu ni mwanariwaya na mwanachama wa Chama Cha Kiswahili cha Kitaifa nchini Kenya, CHAKITA Ken Walibora ameangazia methali isemayo "mtaka unda haneni".
Neno la wiki hii leo tunaangazia methali, baniani mbaya kiatu chake dawa. Mchambuzi wetu ni mwanariwaya na mwanachama wa Chama Cha Kiswahili cha Kitaifa nchini Kenya, CHAKITA Ken Walibora ambaye anasema penye baya hapakosi wema!
Neno la wiki limejikita katika kuichambua methali isema, 'Kijiko cha jikoni, hakiogopi moto'. Mwanariwaya na mwanachama wa Chama Cha Kiswahili cha Kitaifa nchini Kenya, CHAKITA Ken Walibora anasema methali hii kimsingi inaeleza dhana ya kuwa ikiwa mtu ana mazoea fulani au kazoea mazingira fulani, hayamtishi, atatekeleza analolitekeleza bila kuogopa.
Kiswahili kimekuwa na mchango mkubwa kwa wazungumzaji wake hususan Afrika Mashariki kikipigwa jeki na vyombo vya habari kama Radio kwa miaka mingi. Lakini sasa hali ikoje katika kukuza na kuendeleza lugha hii? Ken Walibora ni mwana riwaya na pia amekuwa mwandishi habari akitumia lugha ya Kiswahili miaka nena miaka rudi, Katika mahojiano ,maalum na Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumzia lugha hiyo na jinsi vyombo vya habari vinavyohusika kuiendeleza.
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia neno "Bumbuwazi". Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA .
Bwana Nuhu anasema unapopigwa na butwaa ama kupatwa na mshangao, hadi ukawa huwezi kuongea hata neno moja basi utakuwa umepigwa na bumbuwazi.
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno “Mhanga”, "Manusura" na “Muathirika”. Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Ungana naye upate matumizi sahihi ya maneno hayo..
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno "Mhanga", “Manusura” na "Muathirika". Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Ungana naye upate matumizi sahihi ya maneno hayo..