Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

CDC

Maji safi ya kunywa
World Bank/Arne Hoel

Mradi wa maji wadhibiti kipindupindu DRC 

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa ushirikiano na kituo cha kimarekani cha kudhibiti magonjwa, CDC wamesaidia ujenzi wa tenki za maji kwa ajili ya wakazi wa Kiziba mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na hivyo kusaidia kuepusha maambukizi ya magonjwa yatokanayo na matumizi ya  maji machafu. 

Sauti
2'9"

Magonjwa ya msimu yagharimu maisha ya zaidi ya watu 650,000

Ripoti mpya ya Shirika la afya duniani WHO na kituo cha kudhibiti wa magonjwa cha Marekani, CDC,  imesema  zaidi vifo 650,000 kila mwaka vinahusishwa na magonjwa ya njia ya hewa ikiwemo homa ya mafua inayoambukiza watu nyakati tofauti za misimu.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kuna ongezeko kubwa kutoka idadi ya vifo kati ya 250,000  na 500,000 ndani ya miaka 10 hadi kufikia zaidi ya laki sita vitokanavyo na homa  ya manjano , kisukari, magonjwa ya pumu hususani katika nchi masikini.