Skip to main content

Catherine Russell

Mtoto mwenye umri wa miaka 11 akijipatia ahueni ya joto kali kwa kucheza kwenye chemchem ya maji huko  Uzbekhstan
UNICEF/Pirozzi

Watoto milioni 559 duniani kote wanataabika na joto kali kwa sasa, idadi itaongeza na kufikia zaidi ya bilioni 2 mwaka 2050.

Kuelekea mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP27utakaofanyika nchini Misri barani Afrika, shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya watoto UNICEF wametoa ripoti ya kuonesha athari za mabadiliko ya tabianchi kwa watoto katika kipindi cha kuanzia sasa mpaka mwaka 2050.

© UNICEF/Juan Haro

Walimu wasio na sifa ni moja ya sababu za janga la elimu duniani- UNICEF

Mkutano wa Ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu duniani ukianza leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limetoa taarifa inayoeleza idadi ya Watoto wasiojua kusoma imeongezeka ulimwenguni ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita.Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Assumpta Massoi

Sauti
2'31"
Hivi karibuni, shule moja huko Kharkiv, kaskazini-mashariki mwa Ukraine, iliharibiwa baada ya kushambuliwa kwa makombora. Shule nyingine imeshambuliwa tarehe 7 Mei 2022
© UNICEF/Kristina Pashkina

Shambulio katika shule Ukraine, viongozi UN walaani vikali

Taarifa iliyotolewa hii leo mjini New York Marekani, imeeleza namna Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alivyosikitishwa na shambulio lililoripotiwa tarehe 7 Mei ambalo lilipiga shule huko Bilohorivka, Luhansk nchini Ukraine, ambapo watu wengi walikuwa wakitafuta makazi kutokana na mapigano yanayoendelea.