Kuongezeka kwa ghasia nchini Sudan kunaweka mamilioni ya watoto katika hatari – Mkuu UNICEF
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) Catherine Russell akieleza hii leo kuhusu hali ya watoto nchini Sudan ameeleza kinagaubaga namna hali iliyo hatarishi nchini humo kiasi cha kuwaweka watoto katika hatari kubwa.