Kituo cha ustawi wa jamii Lebanon chaleta nuru kwa mtoto mwenye mkimbizi mwenye usonji
Ingawa Umoja wa Mataifa umekuwa ukipigia chepuo watu wenye matatizo ya usonji wasitengwe wala kuenguliwa kwenye harakati za maendeleo yao, nchini Iraq, hali ni tofauti kwa mtoto Samer mwenye umri wa miaka 10 ambaye ameishi na upweke hadi kituo kimoja nchini Lebanon kilipoleta nuru kwenye maisha yake