Uhalalishaji wa matumizi ya bangi yasiyo ya kitabibu unaweka maisha ya vijana hatarini: INCB
Ripoti mpya ya mwaka 2022 iliyotolewa leo na bodi ya kimataifa ya kudhibiti dawa za kulevya INCB inaonya kwamba kuhalalisha matumizi yasiyo ya kitabibu ya bangi ambayo yanakwenda kinyume na mkataba wa mwaka 1961 wa matumizi ya dawa za kulevya kunaonekana kuongeza kwa kiasi kikubwa matumizi ya dawa hizo na kupunguza uelewa wa hatari zake hususan miongoni mwa vijana.