Chuja:

Canada

Matumizi wa bangi umeongezeka kwa kiasi cha mara nne katika sehemu mbalimbali duniani katika kipindi cha miaka 24 iliyopita.
Unsplash/Wesley Gibbs

Uhalalishaji wa matumizi ya bangi yasiyo ya kitabibu unaweka maisha ya vijana hatarini: INCB

Ripoti mpya ya mwaka 2022 iliyotolewa leo na bodi ya kimataifa ya kudhibiti dawa za kulevya INCB inaonya kwamba kuhalalisha matumizi yasiyo ya kitabibu ya bangi ambayo yanakwenda kinyume na mkataba wa mwaka 1961 wa matumizi ya dawa za kulevya kunaonekana kuongeza kwa kiasi kikubwa matumizi ya dawa hizo na kupunguza uelewa wa hatari zake hususan miongoni mwa vijana.

Esperance Tabisha ajulikanaye pia kama Esperanza akiwa nje ya makazi yao mapya huko Ontario Canada na ni kutokana na programu ya mkimbizi kuhamia nchi ya tatu chini ya mkataba wa kimataifa wa wakimbizi wa mwaka 2018.
UN News Video

Esperance Tabisha: Kutoka kuwa mkimbizi Kakuma hadi mbunifu wa mitindo Canada

Esperance Tabisha, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa ni mnufaika wa mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi, GCR uliopitishwa mwaka 2018 wenye vipengele kadhaa ikiwemo kuhamishia wakimbizi nchi ya tatu. Alikimbia vita DRC na kuingia kambi ya Kakuma nchini Kenya mwaka 2010 na mwaka 2019 akahamia Canada kupitia msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.

19 JULAI 2022

Hii leo jaridani tuna mada kwa kina mahsusi ikimulika raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC aitwaye Esperance Tabisha aliyenufaika na mpango wa Umoja wa Mataifa wa kuhamishia wakimbizi nchi ya tatu kupitia mkataba wa kimataifa wa wakmbizi, GCR. Katoka DRC kaingia kambini Kakuma nchini Kenya na kisha Canada na sasa ni mbunifu wa mitindo akitumia mtandao wa kijamii kupata wateja wake. Janga la COVID-19 lilikuwa chungu na tamu hapo hapo kwa vipi? Thelma anasimulia.

Sauti
12'5"
UNHCR/Gordon Welters

Wakimbizi wakipewa fursa wana mchango katika jamii

Kutana na wakimbizi Bahati Hategekimana kutoka Rwanda, Micheline Muhima kutoka Uganda na Agnes Mude kutoka Sudan Kusini ambao wote walikuwa wakiishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya, lakini sasa kupitia mradi wa majaribio wa kuthamini mchango wa wakimbizi EMPP, unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, mjini Pictou na serikali ya Canada watatu hao si wakimbizi tena bali ni wafanyakazi wa huduma ya jamii kwenye kituo cha Glen Haven Manor kilichopo jimboni Nova Scotia nchini Canada. 

Sauti
2'34"

20 Juni 2022

Jarida hii leo linajikita na siku ya wakimbizi ambapo mwenyeji wako Leah Mushi anaanza na ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ya kwamba kusaka hifadhi ni haki ya msingi ya kila binadamu. Kisha anakupeleka Canada jimboni Nova Scotia ambako wakimbizi kutoka kambini Kakuma nchini Kenya siyo tu wamepata hifadhi bali pia wameajiriwa kupitia mpango maalum wa UNHCR, serikali ya CANADA na shirika la kiraia la kupatia ajira wakimbizi kwenye stadi. Makala ni Iran huko ambako mradi wa kupatia bima wakimbizi umeleta ahueni kwa familia ya mkimbizi mwenye mahitaji makubwa kiafya.

Sauti
9'57"
Kambini Kakuma
UN/Esperanza Tabisha

Wakimbizi tukikirimiwa tunarejesha fadhila kwa jamii:Bahati, Micheline na Agnes

Kutana na wakimbizi Bahati Hategekimana kutoka Rwanda, Micheline Muhima kutoka Uganda na Agnes Mude kutoka Sudan Kusini ambao wote walikuwa wakiishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya, lakini sasa kupitia mradi wa majaribio wa kuthamini mchango wa wakimbizi EMPP, unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, mjini Pictou na serikali ya Canada watatu hao si wakimbizi tena bali ni wafanyakazi wa huduma ya jamii kwenye kituo cha Glen Haven Manor kilichopo jimboni Nova Scotia nchini Canada. 

Sauti
2'34"
Familia ya wakimbizi wa Venezuela wakivuka daraja baina ya Ecuador na Colombia  4 June 2019
© UNHCR/Santiago Escobar-Jarami

UNHCR yaitisha mkutano na wadau kuijadili suluhu ya Venezuela

Venezuela, moja kati ya Mataifa ambayo wananchi wake wanalikimbia kwa wingi takwimu kwenda kuomba hifadhi mataifa mengine ambapo takwimu za hivi karibuni zinaonesha takribani robo ya wananchi wake wamekimbia hali ambayo imeshafanya Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa kuitisha mkutano hii leo kutafuta suluhu ya kudumu. Tuungane na Leah Mushi kwa undani wa taarifa hii

Sauti
2'57"