Jawabu la changamoto za dunia hivi sasa ni mshikamano - Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres siku ya Alhamisi amehutubia mkutano wa viongozi wa kundi la BRICS na kusisitiza umuhimu wa Umoja na Haki katika kutatua changamoto kubwa zinazokumba binadamu hivi sasa kuanzia janga la tabianchi na ukosefu wa usawa kiuchumi hadi mizozo inayotikisa dunia.