Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

BRICS

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (Picha ya maktaba)
United Nations/Cyril Bailleul

HABARI KWA UFUPI: Katibu Mkuu UN ahutubia BRICS. Pia kuna Myanmar vilevile UNICEF na hatima ya watoto Sudan

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amehutubia mkutano wa viongozi kundi la Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini au BRICS huko Johannesburg Afrika Kusini na kusema katika dunia ya sasa iliyogawanyika na kugubikwa na majanga hakuna mbadala mwingine wa kuwezesha kusonga mbele zaidi ya mshikamano hasa kwenye masuala lukuki ikiwemo marekebisho ya mfumo wa kimataifa wa fedha duniani.  

 

Picha na: IAEA

Saratani yasababisha hasara ya dola bilioni 46

Ripoti mpya kutoka katika kituo  cha kimafaida cha utafiti wa ugonjwa wa saratani duniani,IARC inasema ugonjwa huo imezigharimu nchi zenye uchumi wa kati  ,kiasi cha dola za kimarekani bilioni 46 tangu  mwaka 2012.

Katika ripoti hiyo Dkt Alisona Pearce kutoka IARC amesema  nchi hizo zijulikanazo kama BRICS, ambazo  ni China, Brazil, India, Afrika ya kusini  na Urusi ambazo zina idadi ya asilimia 40 ya watu duniani, zinatumia  gharama kubwa katika utafiti na pia matibabu ya ugonjwa wa  saratani, hivyo kuathiri nguvu kazi  na kusababisha hasara kubwa  katika ukuaji wa uchumi.