Mataifa yakishikamana, matumaini na suluhusu vinawezekana:Guterres
Kuanzia migogoro, na matatizo ya kiuchumi, hadi maradhi na mabadiliko ya tabia nchi, changamoto hizi za dunia zinahitaji sasa kuliko wakati mwingine wowote mshikamano imara wa kimataifa, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwaasa viongozi wa dunia kwenye kongamano la kimataifa la Amani lililofanyika leo Jumapili mjini Paris Ufaransa kuadhimisha miaka 100 tangu kumalizika kwa vita ya pili ya dunia.