UNMISS yasaidia mahakama kusikiliza mrundikano wa kesi
Nchini Sudan Kusini ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS unaendelea kuimarisha mfumo wa mahakama ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wote hata maeneo yote ya nchi hiyo.
Nchini Sudan Kusini ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS unaendelea kuimarisha mfumo wa mahakama ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wote hata maeneo yote ya nchi hiyo.
Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS wanafanya kazi ya kuondoa maji ya mafuriko yaliyotwama katika eneo kubwa la mji wa Bentiu jimbo la UNITY ili kuhakikisha uwanja wa ndege na barabara zinazopatakana na uwanja huo zinapitika. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.
Hii leo jaridani tunamulika mwaka mmoja wa watalibani madarakani nchini Afghanistani na madhara yake kwa watoto wa kike. “Watoto wa kike hawaruhusiwi kuendelea na masoko ya elimu ya sekondari.”
Kisha Sudan Kusini ambako walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanahaha kuondoa maji ya mafuriko yaliyotwama kwenye mji wa Bentiu, jimboni Unity.
Makala tunaye kijana Gloria Anderson Mkurugenzi wa shirika la TEDI Tanzania ambalo linahamasisha elimu inayoendana na hali ya sasa ya sayansi na teknolojia ili kuwaandaa wanafunzi kuanzia ngazi za chini kuweza baadaye kujiajiri na kuajiriwa.
Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS wanafanya kazi ya kuondoa maji ya mafuriko yaliyotwama katika eneo kubwa la mji wa Bentiu jimbo la UNITY ili kuhakikisha uwanja wa ndege na barabara zinazopatakana na uwanja huo zinapitika.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo inaonyesha ongezeko la ukatili wa kingono katika jimbo la Unity kaskazini mwa Sudan Kusini, ikisema wanawake 134 na wasichana wamebakwa na wengine 41 wamekumbwa na aina nyingine za ukatili wa kingono kati ya Septemba na Disemba 2018.
Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika, AU wametoa taarifa ya pamoja ya maelezo yao juu ya kuchukizwa na na visa vya ukatili wa kingono, ikiwemo kubakwa, vilivyotekelezwa dhidi ya wanawake na wasichana takriban 150 karibu na mji wa Bentiu nchini Sudan Kusini mwishoni mwa mwezi uliopita.
Wachunguzi wa masuala ya haki za binadamu wanamiminika huko Bentiu nchini Sudan Kusini kuchunguza madai ya visa vya kubakwa kwa wanawake na wasichana 150 kwa siku 10 mwishoni mwa mwezi uliopita.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan kusini UNMISS umelaani vikali mfululuzo wa mashambulizi ya ukatili wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana waliokuwa wakisafiri kutoka vijijini kwao kuelekea Bentiu kwenye jimbo la Unity.
Amani ya kudumu na endelevu haitopatikana nchini Sudan Kusini endapo jamii hususan wanawake hawatoshirikishwa katika mchakato wa kuileta. Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa operesheni za ulinzi wa Umoja wa Mataifa Jean Pierre Lacroix baada ya kukutana na wanawake wakimbizi wa ndani kwenye eneo la Bentiu nchini humo.
Utapiamlo uliokithiri sasa ukumba tu siyo watu wazima bali pia watoto. Sasa wanaishi kwa kula mabua na mianzi porini.