Skip to main content

Chuja:

Barubaru

Mtoto akitabasamu darasani wakati wa ziara ya pamoja ya ECW na Norway kwenye maeneo nufaika ya miradi ya elimu inayofadhiliwa na pande mbili hizo.
ECW

Watoto milioni 222 walio katika maeneo yaliyoathirika na migogoro wanahitaji msaada wa haraka wa elimu:ECW 

Mfuko wa Umoja wa Mataifa unaohusika na kusongesha elimu kwenye maeneo yenye majanga na mizozo ya muda mrefu, Education Cannot Wait, ECW au kwa lugha ya Kiswahili, Elimu Haiwezi Kusubiri, pamoja na wadau wamesisitiza umuhimu wa kusaidia mamilioni ya watoto walio katika mazingira ya migogoro ili waweze kupata elimu, wakisema elimu ndio ufunguo wa kuwakomboa watoto hao hususan wasichana katika maisha yao ya siku za usoni.

Sauti
3'7"
Takriban thuluthi moja ya wanawake wote katika nchi zinazoendelea huanza kuzaa wakiwa na umri wa miaka 19 na kushuka chini ya umri huo.
UNFPA/Thalefang Charles

Karibu theluthi ya wanawake wote katika nchi zinazoendelea wanajifungua wangali vigori:UNFPA

Matokeo ya utafiti mpya wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani na masuala ya afya ya uzazi UNFPA yaliyotolewa leo yanaonesha kuwa karibu theluthi moja ya wanawake wote katika nchi zinazoendelea wanaanza kupata Watoto wakiwa na umri wa miaka 19 au chini ya hapo, na karibu nusu ya uzazi wote wa mara ya kwanza wa barubaru huwa ni wa Watoto au wasichana wa umri wa miaka 17 au chini ya hapo. 

24 Novemba 2021

karibu kusikiliza jarida hii leo Flora Nducha anakuletea mada kwa kina maalum ikiwa ni kelele cha wiki ya kukuza uelewa kuhusu viuajiumbemaradhi, utasikia ushiriki wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula. 

Kabla ya mada hiyo kwa kina utasikia habari kwa ufupi zikiangazia masuala ya COVID-19 ambapo taarifa zinaonesha maambukizi yameendelea kuongezeka hususan barani ulaya lakini barani Afrika yamepungua. 

Pia utasikia kuhusu chanjo ya COVID-19 kwa watoto na Barubaru pamoja na wito uliotolewa kwa nchi zote duniani kuhusu usawa wa kijinsia. 

Karibu. 

Sauti
12'33"
Mfanyakazi wa ndani kutoka  makazi ya Kalayanpur nchini Bangladesh amepoteza kazi sababu ya janga la COVID-19
WFP/Sayed Asif Mahmud

WHO inachunguza hatari za maambukizi ya COVID-19 kwa watoto na barubaru

Wakati idadi ya wagonjwa wa corona au COVID-19 waliothibitishwa au kukutwa na virusi miongoni mwa watoto imefikiwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa tangu kuzuka kwa janga hilo na tangu kuanza kwa muhula mpya wa masomo katika nchi mbalimbali, shirika la afya duniani WHO linaamini kuwa aina mpya ya virusi vya Corona inaonekana kuwagusa zaidi vbarubaru. 

UNICEF/Henry Bongyereirwe

Hakuna uzuri wowote wakushiriki ngono katika umri mdogo

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto -UNICEF nchini Uganda linafadhili mradi wa Mama kwa Mama ambao unajengea uwezo maafisa wa ustawi wa jamii wanaopita kila kaya maskini kusaka  barubaru na vijana balehe waliopata mimba katika umri mdogo na kuwapatia stadi za ufundi ili  hatimaye waweze kujipatia kipato na kubadilisha maisha yao. 
(Taarifa ya Leah Mushi) 
 

Sauti
1'52"
Shirika la afya duniani WHO linawachagiza vijana barubaru kufanya mazoezi ya viungo na zaidi kwa ajili ya afya na mustakabali wao
Unsplash/Paul Proshin

Hakuna faida ya kungonoka mapema- Kijana balehe

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto -UNICEF nchini Uganda linafadhili mradi wa Mama kwa Mama ambao unajengea uwezo maafisa wa ustawi wa jamii wanaopita kila kaya maskini kusaka  barubaru na vijana balehe waliopata mimba katika umri mdogo na kuwapatia stadi za ufundi ili  hatimaye waweze kujipatia kipato na kubadilisha maisha yao

Sauti
1'52"
UN Photo/Eskinder Debebe)

Mradi wa UNICEF Liberia wadhihirisha uwezo wa barubaru katika kubadili maisha yao

Nchini Liberia, mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF wa kuboresha maisha ya wasichana barubaru umekuwa na mchango mkubwa katika kushirikisha kundi hilo kwenye harakati za kuinua jamii zao na wakati huo huo kurejea shuleni. Ahimidiwe Olotu na maelzo zaidi.

Kutana na Hawa Wanita Page (Pegh) mratibu wa mradi wa UNICEF kuhus barubaru nchini Liberia.

Sauti
1'33"