Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Baraza la usalama la umoja wa mataifa

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto kwenye maeneo ya mizozo, Virginia Gamba amewasilisha ripoti ya mwaka ya Katibu Mkuu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
UN Photo/Eskinder Debebe

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lajadili ripoti ya mwaka 2021 ya watoto katika maeneo yenye mizozo

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wake wa mwaka kuhusu watoto kwenye maeneo yenye mizozo ambapo Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto hao, Virginia Gamba amewasilisha ripoti ya mwaka ya Katibu Mkuu ambayo iliwekwa bayana kwa umma tarehe 11 mwezi huu wa Julai ikitaja aina sita ya vitendo vibaya zaidi vya ukiukwaji dhidi ya watoto. 

Soko nchini Sudan Kusini
© UNICEF/Sebastian Rich

Vikwazo bado ndio njia japo inabidi kuangaliwa kupunguza matokeo mabaya- DiCarlo 

Naibu Katibu Mkuu wa Masuala ya Kisiasa na Amani, Rosemary A. DiCarlo, leo Februari 7 ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba "vikwazo vinasalia kuwa chombo muhimu cha Mkataba kilichopo kwa Baraza ili kuhakikisha udumishaji wa amani na usalama wa kimataifa, "lakini akasisitiza kuwa" mengi zaidi yanaweza kufanywa ili kupunguza matokeo mabaya yanayoweza kutokea” ya vikwazo hivi. 

Katibu Mkuu António Guterres akihutubia mkutano wa Baraza la Usalama kuhusu Kutengwa, kukosekana kwa usawa na migogoro chini ya kudumisha amani na usalama wa kimataifa.
UN Photo/Eskinder Debebe)

Kuzuia migogoro ni kiini cha amani ya kudumu :Guterres

Kuzuia migogoro ndio nguzo kuu ya kuhakikisha amani ya kudumu duniani amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizungumza kwenye mjadala wa wazi wa Baraza la Usalama hii leo mjini New York Marekani uliojikita katika mada ya “amani na usalama kupitia njia za kidiplomasia za kuzuia migogoro.”