Mkutano wa ngazi za juu wa ”Afrika tuitakayo” wafanyika Makao Makuu ya UN
Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kumefanyika mkutano wa ngazi za juu maalum kuangazia masuala ya maendeleo barani Afrika.
Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kumefanyika mkutano wa ngazi za juu maalum kuangazia masuala ya maendeleo barani Afrika.
Leo tarehe 21 Septemba mwaka 2021 ni siku ya amani duniani halikadhalika siku ya kwanza ya mjadala mkuu wa mikutano ya ngazi ya juu ya Umoja wa Mataifa katika makao makuu ya UN nchini Marekani.
Karibu Usikilize Jarida ambapo utasikia mengi kuhusu #UNGA76
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo amezichagiza nchi wanachama kuhimiza hatua za pamoja katika kupambana na janga la corona au COVID-19 katika kikao cha kwanza cha ana kwa ana tangu mwezi Machi mwaka huu.
Tukielekea wiki ya vikao vya mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa vitakavyowakutanisha viongozi wa dunia katika makao makuu ya umoja huo mjini New York Marekani kuanzia jumatatu ya wiki ijayo, Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Modest Mero amezungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa na kueleza kuwa mijadala ya viongozi wakuu wa dunia itatawaliwa na changamoto kuu tano ambazo dunia nzima inakabiliana nazo hivi sasa.
Ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo Alhamisi uligubikwa na maneno ya vijembe wakati wawakilishi wa nchi 193 wanachama wa Umoja huo walipokuwa wanatoa maoni yao kabla ya kupiga kura ya kutaka Marekani ibadili uamuzi wake wa kutambua Yerusalem kama mji mkuu wa Israel. Flora Nducha na ripoti kamili.
(Taarifa ya Flora Nducha)
Je Yerusalem utakuwa au ni mji mkuu wa Israel?
Ni sakata lililotawala baraza kuu la umoja wa Mataifa hii leo katuika kikao cha dharura mjini New york Marekani.
Kila mwamba ngozi akivutia kwake..