Skip to main content

Chuja:

Banice Mbuki Mburu

Walinda amani wa Umoja wa MAtaifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO wamesherehekea siku ya walinda amani duniani kwa kutembelea kituo cha watoto yatima huko Oicha jimboni Kivu Kaskazini.
UN News/George Musubao

DRC: Walinda amani wa UN kutoka Tanzania washerehekea siku yao kwa kutembelea watoto

Kikosi cha 10 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANZBATT-10 kinachohudumu kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi (FIB) kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kimeadhimisha siku ya ulinzi wa amani duniani hii leo tarehe 29 Mei kwa kutembelea kituo cha watoto yatima cha DORIKA kilichopo OICHA Jimbo la Kivu kaskazini nchini DRC. Wakiwa kituoni hapo wamewapatia misaada ya kiutu watoto hao ikiwa pia ni lengo la kulinda uhusiano na ushirikiano kwenye eneo lao hilo la uwajibikaji.

Takriban watu milioni 2 hadi milioni 2.5 wanatarajiwa kutumbukia kwenye janga la njaa nchini Sudan katika miezi michache ijayo.
© WFP/Peter Louis

Kuna hatari ya kuongezeka njaa - yaonya ripoti mpya ya UN 

Ripoti - 'Maeneo yenye Njaa - FAO-WFP onyo la mapema juu ya uhaba mkubwa wa chakula' - iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula (WFP) inataka hatua za haraka za kibinadamu kuokoa maisha na njia za kujikimu na kuzuia njaa na vifo katika maeneo yenye njaa kali ambayo iko katika hatari kubwa ya kuongezeka kuanzia Juni hadi Novemba 2023.

Pichani, Isatou, Mariama na Fatoumatta hawalazimiki tena kutoenda shule wakati wa hedhi baada ya UNFPA kusaidia uzalishaji na mgao wa bure wa taulo za kike zitumikazo tena na tena wa ajili ya shule ikiwemo shule yao ya viziwi mjini Banjul, Gambia.
UNFPA Gambia

Afya ya hedhi ni suala la haki za binadamu sio tu la kiafya

Leo ni siku ya usafi wa hedhi, kauli mbiu ya siku hii ni "Kufanya hedhi kuwa jambo la kawaida la maisha ifikapo mwaka 2030."

Siku hii huadhimishwa kila tarehe 28 ya mwezi wa Mei kila mwaka kwa sababu mizunguko ya hedhi ni wastani wa siku 28 na watu hupata hedhi wastani wa siku tano kila mwezi.