Skip to main content

Chuja:

Baidoa

Photo: UNICEF/Athanas Makundi

Mashirika ya UN yahaha kuwasaidia waathirika wa mizozo na ukame Baidoa Somalia

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO linasema idadi ya milipuko ya magonjwa iliyoripotiwa na pia dharura za kiafya zinazohusiana na tabianchi katika Ukanda wa Pembe ya Afrika zimefikia kiwango cha juu zaidi kuwahi kutokea karne hii, na hivyo kuzidisha janga la kiafya katika eneo ambalo watu milioni 47 tayari wanakabiliwa na njaa kali. Mfano wa hivi karibuni ni katika maeneo kadhaa ya Pembe ya Afrika kama Somalia.

Sauti
4'27"
Ismail Isack Amin, mkulima mwenye umri wa miaka 66 ambaye anasema amekuwa akijinufaisha na ardhi  yenye rutuba nchini mwake Somalia tangu akiwa na umri wa miaka
UNSOM video screen capture

Ardhi imesalia kuwa mkombozi wangu- Mkulima Somalia

Nchini Somalia, harakati za kuhakikisha wananchi wanashiriki kwenye shughuli za kiuchumi na kijamii zinaendelea kuzaa matunda kwa wananchi ambapo ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini  humo, UNSOM inadhihirisha juhudi hizo kupitia mfululizo wa video zinazonesha wananchi wakishiriki harakati mbalimbali.