Nusu ya watu duniani watakuwa katika hatari ya mafuriko, vimbunga na Tsunami ifikapo 2030:UN
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu Tsunami Umoja wa Mataifa umeonya kwamba kufikia mwaka wa 2030, inakadiriwa kuwa asilimia 50 ya watu wote duniani wataishi katika maeneo ya pwani ambayo yanakabiliwa na mafuriko, vimbunga na tsunami.