Mwaka 2019 unashikilia rekodi ya joto kali duniani baada ya 2016:WMO
Shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO leo limesema mwaka 1029 unashikilia rekodi ya pili ya kuwa wenye joto Zaidi duniani ukiacha mwaka 2016.
Shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO leo limesema mwaka 1029 unashikilia rekodi ya pili ya kuwa wenye joto Zaidi duniani ukiacha mwaka 2016.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Australia limetuma salamu zake za masikitiko kwa watoto na familia zilizoathirika na janga la moto linaloendelea kote nchini Australia.
Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, hii leo mjini Geneva Uswisi wameisihi Australia kuwapatia kwa haraka huduma ya afya wasaka hifadhi zaidi ya 800 na wahamiaji wengine ambao wamekuwa wakishikiliwa katika kambi zilizoko katika fukwe za nchi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano bila suluhisho.
Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya faragha Joe Cannataci amesema amepokea taarifa leo asubuhi za kukamatwa kwa Julian Assange mjini London Uingereza na akafafanua kwamba “hili halitozuia juhudi zangu za kutathimini madai ya bwana Assange kwamba haki yake ya faragha imekiukwa.”
Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na UKIMWI -UNAIDS, umekaribisha mchango wa nyongeza wa zaidi ya dola 977,000 kwa ajili ya harakati zake za kupambana na ugonjwa huo.