Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

athari za mazingira

Viwanda vidogovidogo vyalaumiwa kuchafua vyanzo vya maji

Maji safi na salama ni uhai wa viumbe vyote ulimwenguni ikijumuisha binadamu, wanyama na mimea. Lengo namba 6 la  malengo ya maendeleo  endelevu, SGD linazungumzia maji safi na salama kwa kila mtu ifikapo  ya mwaka 2030.

Katika migogoro ya kimazingira, viwanda vidogo na vikubwa vimekuwa vikilalamikiwa kuharibu mazingira kwa kujenga mifereji inayopeleka maji taka katika vyanzo vya maji au mito.

Sauti
3'55"

Saidieni kupambana na uharibifu wa mazingira: Guterres

Tuna haki ya kuishi sehemu salama, tunategemea kula chakula bora, maji safi na kuvuta hewa safi lakini bado tunaendelea kuharibu mazingira.

Huo ni ujumbe wa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika mkutano mkuu wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa unaofanyika Nairobi, Kenya.

Guterres amesema tayari kuna mbinu na maazimio madhubuti za kupambana na mabadiliko ya tabia nchi yanayoweza kuigwa kuinusuru dunia isiendelee kuathirika.