Vijana endeleeni kupaza sauti kuokoa mazingira- Guterres
Wakati janga la tabianchi tayari likiwa limeleta madhara kwa maisha na vipato va watu kote ulimwenguni, vijana watakuwa na nafasi muhimu zaidi katika kusongesha mbele hatua mujarabu, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake kwa vijana wanaoshiriki mkutano tangulizi wa COP-26 huko mjini Milano nchini Italia.