Skip to main content

Chuja:

António Guterres 

Mkutano wa Kubadilisha Elimu uliitishwa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa huko New York mnamo 2022.
UN Photo/Cia Pak

Kazi na dhamira ya UN ni muhimu zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote: Guterres

Katika dunia inayokabiliwa na changamoto zinazozidi kuwa ngumu kuanzia umaskini na ukosefu wa usawa hadi dharura ya mabadiliko ya tabianchi, Umoja wa Mataifa unaendelea kuwa mstari wa mbele katika kukabiliana na changamoto hizo za dunia, ukiwa na nia ya kuuweka ubinadamu kwenye njia ya amani na ustawi, amesema Katibu Mkuu wa umoja wa Mataifa António Guterres.

Watu wakiandamana kupinga silaha za nyuklia katika  mkutano wa mabadiliko ya tabianchi huko Geneva. (maktaba)
ICAN/Lucero Oyarzun

UN yataka kila nchi itie saini kutofanya majaribio ya silaha za nyuklia

Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kupinga majaribio ya silaha za nyuklia Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Csaba Kőrösi amesema kitendo cha matumizi ya kijeshi duniani kufikia dola trilioni 2.2 mwaka 2022 si ishara nzuri kwa usalama wa dunia na kutoa wito wa utashi wa kisiasa kwa nchi zote katika kuhakikisha dunia haina matumizi ya silaha za nyuklia. 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres
UN Photo/Mark Garten

UN yaendelea kufuatilia kinachoendelea Iran

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anafuatilia kwa karibu maandamano yanayoendelea nchini Iran ambayo chanzo chake ni kifo cha msichana Mahsa Amini aliyekufa mikononi mwa polisi baada ya kukamatwa tarehe 13 Septemba kwa madai ya kuvaa hijabu kinyume na inavyotakiwa nchini humo.

Mwaka 2010, Malkia wa Elizabeth wa II wa Uingereza akiweka shada la maua kwenye eneo la kukumbuka watumishi wa UN waliopoteza maisha yao wakihudumia shirika.
UN /Evan Schneider

Tumuenzi Malkia Elizabeth kwa kufanya kazi kwa bidii ili tuwe UN ya kweli- Katibu Mkuu

Jua limezama kwa mtawala wa aina yake! Ndivyo alivyoanza hotuba yake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo kwenye ukumbi wa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani, ambamo wawakilishi wa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa walikutana katika tukio maalum la kuenzi Malkia Elizabeth wa II wa Uingereza aliyega dunia tarehe 8 mwezi huu wa Septemba huko Scotland.

Katibu Mkuu António Guterres (kushoto) alishuhudia athari za mafuriko katika majimbo ya Sindh na Balochistan. Akiwa huko, alikutana na watu walioathiriwa na mafuriko, pamoja na mashirika ya kiraia na watu waliofika mwanzo kusaidia.
UN Photo/Eskinder Debebe

Katibu Mkuu wa UN ashuhudia kiasi cha juu cha uvumilivu na ushujaa Pakistani 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, alipokuwa akihitimisha zaiara yake ya siku mbili nchini Pakistani Jumamosi ya Septemba 10, amesisitiza kwamba mahitaji katika Pakistan iliyokumbwa na mafuriko ni makubwa na akatoa wito wa msaada mkubwa na wa haraka wa kifedha, alipokuwa akihitimisha safari ya siku mbili yenye lengo la kuongeza ufahamu wa maafa yanayotokana na taianchi, anaripoti Shirin Yaseen wa UN News ambaye ni miongoni mwa waliosafiri na Katibu Mkuu.