Kazi na dhamira ya UN ni muhimu zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote: Guterres
Katika dunia inayokabiliwa na changamoto zinazozidi kuwa ngumu kuanzia umaskini na ukosefu wa usawa hadi dharura ya mabadiliko ya tabianchi, Umoja wa Mataifa unaendelea kuwa mstari wa mbele katika kukabiliana na changamoto hizo za dunia, ukiwa na nia ya kuuweka ubinadamu kwenye njia ya amani na ustawi, amesema Katibu Mkuu wa umoja wa Mataifa António Guterres.