04 AGOSTI 2023
Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu na Akili Mnemba au ‘Artificial Intelligence’. Makala tunakupeleka nchini Brazil na mashinani tutasikia ujumbe wa kijana kutoka Tanzania, salía papo hapo!
Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu na Akili Mnemba au ‘Artificial Intelligence’. Makala tunakupeleka nchini Brazil na mashinani tutasikia ujumbe wa kijana kutoka Tanzania, salía papo hapo!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo tunaangazia afya ya uzazi na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya afya ya uzazi salama kwa wanawake kutoka hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Dk. Elieza Chibwe akizungumzia juu ya kukoma kwa hedhi kwa wanawake anasema “Ukihisi dalili za menopause mapema nenda hospitali.” Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo salamu za sikukuu za Pasaka na Eid El Fitr kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ombi la UNICEF la msaada kwa watoto waathirika wa matetemeko ya ardhi huko mashariki ya kati, na haki za watu wa jamii asili.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amefanya ziara nchini Iraq lengo likiwa ni kusisitiza mshikamano na kuunga mkono juhudu za nchi za kuleta amani ,haki za binadamu na maendeleo endelevu.
Ziara ya mwisho ya Katibu Mkuu Guterres nchini Iraq ilikuwa miaka sita iliyopita, na alipofika Baghdad alipokelewa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya nje Fued Hussein ambapo walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari.
“Kila Mwaka Mpya ni wakati wa kuzaliwa upya”, ndivyo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres alivyozianza salamu za mwaka mpya wa 2023 kwenda kwa ulimwengu.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya jamii za asili, dunia imehimizwa kuonesha mshikamano wa kweli na kufanya kazi kwa pamoja katika kuhakikisha kunakuwa na usawa kwa watu wa asili, kutambua dhuluma wanazovumilia, na kusherehekea maarifa na hekima zao.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ameelezea kusikitishwa na ripoti za raia kuuwawa na wengine kutekwa na kundi la watu waliojihami kaskazini mwa jimbo la Borno kwenye eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria
Tatizo la wakimbizi ni jukumu la kila mtu sio wakimbizi au nchi zinazowahifadhi pekee, kwani nimejifunza ukarimu sio lazima uendane na utajiri. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hii leo katika kongamano la kimatifa kwa ajili ya wakimbizi linaloendelea mjini Geneva Uswis.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amepokea tuzo ya Charlemangne huko mjini Aachen nchini Ujerumani na kusema kuwa ni heshima kubwa sana kwake.
Ushirika wa Kusini-Kusini ni muhimu sana katika vita vya kimataifa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo Jumatano kwenye ufunguzi wa mkutano wa pili wa Umoja wa Mataifa kuhusu ushirika wa Kusini-Kusini unaoendelea mjini Buenos Aires nchini aregentina.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo akihutubia mkutano maalumu unaofanyika mjini Geneva Uswisi kuhusu udhibiti wa silaha amesema maono mapya ya kimataifa ya udhibiti wa silaha yanahitajika na nchi hazipaswi "kulala" katika mbio mpya ya silaha za nyuklia.