Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Annalena Baerbock

UN News/Abdelmonem Makki

Akiwa Doha, Rais wa Baraza Kuu aona watoto wa kipalestina walivyo na matumaini licha ya zahma walizopita

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Annalena Baerbock ametembelea wakimbizi wa kipalestina huko Doha nchini Qatar kuwajulia hali na kujionea maisha yao baada ya kuondolewa wakati wa vita kali huko Ukanda wa Gaza eneo la wapalestina linalokaliwa kimabavu na Israel na kuletwa nchini Qatar kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Leah Mushi anatupa taswira ya ziara yake hiyo.

Sauti
4'6"
 Annalena Baerbock alipowahutubia waandishi wa habari katika Umoja wa Mataifa baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa UNGA80 mwezi Juni 2025.
UN Photo/Eskinder Debebe

Annalena Baerbock aapa kushika usukukani wa Urais wa UNGA80

Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA79 umefikia tamati hii leo na kupisha Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA80 ambao nao utadumu kwa mwaka mmoja chini ya uongozi wa Rais mpya Annalena Baerbock. Bi. Baerbock ambaye ni raia wa Ujerumani anakuja na kauli mbiu inayosema, “Tutakuwa Bora Tukishikamana.”