Huduma ya kibinadamu ni wito-Wakili Kamunya
Kutoa huduma ya kibinadamu iwe ni katika mazingira yoyote yale ni wito ambao ni lazima utoke moyoni amesema Ann N. Kamunya wakili mtetezi wa haki za wanawake, raia wa Kenya ambaye sasa yuko Ankara, Uturuki akifanya kazi za huduma za kibinadamu na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.