04 AGOSTI 2023
Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu na Akili Mnemba au ‘Artificial Intelligence’. Makala tunakupeleka nchini Brazil na mashinani tutasikia ujumbe wa kijana kutoka Tanzania, salía papo hapo!
Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu na Akili Mnemba au ‘Artificial Intelligence’. Makala tunakupeleka nchini Brazil na mashinani tutasikia ujumbe wa kijana kutoka Tanzania, salía papo hapo!
Hii leo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu amani na usalama duniani likimulika fursa na hatari zitokanazo na Akili Mnemba au Akili Bandia, AI ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesihi Baraza hilo lioneshe uongozi katika nyanja hiyo hasa katika kuhakikisha teknolojia hiyo inatumika kujenga madaraja ya kijamii, kidijitali na kiuchumi badala ya kuleta utengano na uharibifu.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Eugene Uwimana mmoja wa maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini Rwanda amemtembelea mhamasishaji wa lugha ya Kiswahili nchini humo Profesa Pacifique Malonga ambaye ameanzisha eneo maalumu la vitabu vya Kiswahili katika Maktaba Kuu ya mji wa Kigali. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za uhamiaji, usafirishaji haramu wa binadamu na Akili Bandia. Katika jifunze Kiswahili hii leo tunabisha hodi kwenye Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA kupata ujumbe maalum kuhusu umuhimu wa lugha.
Uundaji wa akili bandia, au AI, kwa faida ya wote unahitaji njia za ulinzi zinazozingatia haki za binadamu, uwazi na uwajibikaji, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo leo inaturejesha hapa Makao makuu ya umoja wa Mataifa kusiki maandalizi ya maadhimisho ya pili ya siku ya Lugha ya Kiswahili duniani. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo ripoti ya Katibu Mkuu kuhusu watoto katika migogoro ya silaha, msaada kwa wakimbizi nchini Sudan na maadili ya akili bandia. Katika mashinani tunakupeleka nchini Mali, kulikoni?
Nchi lazima zishughulikie “madhara makubwa duniani” yanayosababishwa na kuenea kwa chuki na uongo mtandaoni, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo wakati akizindua ripoti muhimu iliyoundwa ili kuimarisha uadilifu wa habari kwenye majukwaa ya kidijitali.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO limeanzisha mchakato wa kujadili fursa, changamoto na hatari za mifumo zalishi ya akili bandia katika mifumo ya elimu duniani.
Ili kukabiliana na uibukaji wa kasi na mpya wenye nguvu wa akili bandia (AI) shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni UNESCO limefanya mkutano wa kwanza wa kimataifa wa Mawaziri wa Elimu ili kuchunguza fursa za sasa na zijazo, changamoto na hatari ambazo AI inaweza kuleta kwenye mifumo ya elimu.
Kamishna Mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk ameeleza kusikitishwa sana na uwezekano wa madhara kutokana na maendeleo ya hivi karibuni katika akili bandia (AI)
Miongoni mwa yaliyomo
Kujaa maji kwa ziwa Albert nchini Uganda kwaleta zahma kubwa kwa wakazi, wengine wapoteza makazi, Umoja wa Mataifa nao wanyoosha mkono kusaidia.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres asema kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya viwango vya chini vya wanawake wanaofanya kazi katika masuala ya Akili Bandia (AI), na kanuni za hovyo za upendeleo wa kijinsia.