Mtu 1 anauawa kwenye ajali barabarani katika kila sekunde 24- UN
Kila sekunde 24 mtu mmoja anakufa kwenye ajali ya barabarani! Ndivyo ulivyoanza ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika maadhimisho ya leo ya siku ya kukumbuka waliopoteza maisha au kujeruhiwa kutokana na ajali za barabarani.