Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Agenda 2030

Hapa ni kwenye moja ya soko nchini Thailand, wadudu wakiuzwa kama kitoweo.
P.B. Durst

Utamaduni na chakula ni chachu ya kutimiza SDGs:UNESCO

Kongamano la kimataifa lililoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataoifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO limeanza leo mjini Parma Italia likimulika jinsi gani chakula na utamaduni vinavyoweza kutoa suluhu ya changamoto zinazoikabili dunia za ongezeko la idadi ya watu duniani, mabadiliko ya tabianchi na jukwaa kwa ajili ya majadiliano ya jamii jumuishi. 

Sauti
2'1"
Washiriki wa CSW63 wakisherehekea kukamilika kwa mkutano huo mjini New York Marekani.
UN Women/Ryan Brown

CSW63 yakunja jamvi kwa mkakati kuwahakikishia wanawake ulinzi, usalama na fursa za kiuchumi.

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na kukuza usawa wa kijinsia na kuwaezesha wanawake, UN Women limehitimisha mkutano wake wa mwaka mwishoni mwa wiki hii mjini New York Marekani kwa makubaliano kuhusu njia za kulinda na kuboresha jinsi wasichana na wanawake watakavyoweza kufikia mifumo ya ulinzi wa kijamii, huduma za kijamii na miundombinu endelevu.