Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Afya ya uzazi

Mshauri wa kike anamuonyesha mwanamke njia za kupanga uzazi katika kituo cha afya huko Sulawesi Kusini, Indonesia.
© UNICEF/Shehzad Noorani

WHO waboresha kitabu cha muongozo wa uzazi wa mpango

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO hii leo limetoa maboresho muhimu kwenye Kitabu chake cha kihistoria cha Uzazi wa mpango, ambacho kinawapa watunga sera na wafanyakazi wa sekta ya afya taarifa mpya za kuweza kufanya machaguo kuhusu dawa za uzazi wa mpango.

25 OKTOBA 2022

Hii leo kwenye Jarida la Umoja wa Mataifa tunakuletea mada kwa kina ikimulika filamu ya chapa tatu iliyotengenezwa na taasisi ya Tai Tanzania kuhusu haki za binadamu yeyote yule wakiwemo watu wenye ualbino, Mtoto Njaro ana uwezo mkubwa wa ubunifu, anakutana na changamoto kwenye jamii yake lakini hakati tamaa, anasonga mbele hadi anaibuka mshindi.

Kuna habari kwa ufupi kutoka kwake Flora Nducha akimulika:

Sauti
12'48"
Takriban thuluthi moja ya wanawake wote katika nchi zinazoendelea huanza kuzaa wakiwa na umri wa miaka 19 na kushuka chini ya umri huo.
UNFPA/Thalefang Charles

Karibu theluthi ya wanawake wote katika nchi zinazoendelea wanajifungua wangali vigori:UNFPA

Matokeo ya utafiti mpya wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani na masuala ya afya ya uzazi UNFPA yaliyotolewa leo yanaonesha kuwa karibu theluthi moja ya wanawake wote katika nchi zinazoendelea wanaanza kupata Watoto wakiwa na umri wa miaka 19 au chini ya hapo, na karibu nusu ya uzazi wote wa mara ya kwanza wa barubaru huwa ni wa Watoto au wasichana wa umri wa miaka 17 au chini ya hapo. 

Ukosefu wa taarifa au uelewa kuhusu ngono na afya ya uzazi umechangia msichna wa miaka 18 kupata mimba isiyo tarajiwa huko Timor Leste
© UNFPA/Ruth Carr

Nusu ya mimba zote duniani hazikutarajiwa: UNFPA

Ripoti ya Hali ya Idadi ya Watu Duniani mwaka 2022, iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA inasema karibu nusu ya mimba zote, ambazo ni jumla ya milioni 121 kila mwaka duniani kote, hazikutarajiwa. 

23 MACHI 2022

Katika Jarida la Jumatano Machi 23, 2022 kuna habari kwa ufupi zilkilenga mateso yanawowakibili wanawake wakati wa kujifungua, ujumbe wa Katibu Mkuu katika siku ya utabiri wa hali ya hewa duniani na wito wa ILO kwa Russia kukomesha uvamizi Ukraine pia  tunaangazia kikao cha 66 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani kinachoendelea hapa Makao makuu ya Umoja wa Mataifa na hususan hatua zilizopigwa na Tanzania katika kusongesha usawa wa kijinsia, kwenye mashinani tutasikia kuhusu msaada linalotoa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi UNHCR nchini Poland.

Sauti
12'39"

3 Machi 2022

Jaridani hii leo Leah Mushi anaanzia huko Ukraine ambako mashambulizi yanayoaendelea yanahatarisha afya ya uzazi ya wanawake na watoto wa kike. Kisha anamulika siku  ya kimataifa ya wanyapori akiangazia ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kutaka kuendelea kulindwa kwa wanyamapori kwa maslahi ya binadamu na sayari duniani. Suala la uwezeshaji wanawake kiuchumi linamulikwa pia kwa kubisha hodi Kigoma nchini Tanzania ambako Umoja wa Mataifa kupitia FAO unawapa wanawake uwezo wa kujiamini kupitia kilimo cha maharage.

Sauti
13'25"