WHO waboresha kitabu cha muongozo wa uzazi wa mpango
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO hii leo limetoa maboresho muhimu kwenye Kitabu chake cha kihistoria cha Uzazi wa mpango, ambacho kinawapa watunga sera na wafanyakazi wa sekta ya afya taarifa mpya za kuweza kufanya machaguo kuhusu dawa za uzazi wa mpango.