Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Afya ya uzazi

03 OKTOBA 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na inatupeleka Kibokoni, Kaunti ya Kilifi nchini Kenya ambako mabwawa ya samaki yamebadili kabisa maisha ya wavuvi wa eneo hilo walioathirika na mabadiliko ya tabianchi yaliyosabisha samaki kutoweka baharini na kuwakatisha tamaa ya Maisha. Lakini sasa kupitia mradi wa ufugaji samaki ulio chini ya mwamvuli wa Umoja Self-Help Group jamii hiyo ina mabwawa 17 ya samaki yanayozalisha samaki aina ya milkfish, kamba, kaa, sandfish, rabbitfish na perege au tilapia. Mshiani tanakuletea ujumbe kusu afya ya uzazi na uswa wa kijinsia. 

Sauti
11'35"
Pichani, Isatou, Mariama na Fatoumatta hawalazimiki tena kutoenda shule wakati wa hedhi baada ya UNFPA kusaidia uzalishaji na mgao wa bure wa taulo za kike zitumikazo tena na tena wa ajili ya shule ikiwemo shule yao ya viziwi mjini Banjul, Gambia.
UNFPA Gambia

Afya ya hedhi ni suala la haki za binadamu sio tu la kiafya

Leo ni siku ya usafi wa hedhi, kauli mbiu ya siku hii ni "Kufanya hedhi kuwa jambo la kawaida la maisha ifikapo mwaka 2030."

Siku hii huadhimishwa kila tarehe 28 ya mwezi wa Mei kila mwaka kwa sababu mizunguko ya hedhi ni wastani wa siku 28 na watu hupata hedhi wastani wa siku tano kila mwezi.

11 MEI 2023

Jaridani hii leo tunakuletea mada kwa kina ikimulika harakati za shirika moja la kiraia huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC za kuitikia wito wa Umoja wa Mataifa wa kuona mitandao ya kidijitali inatumika kuimarisha afya hasa ya wajawazito na watoto. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Sudan na Afghanistan, na changamoto za utoaji wa msaada wa chakula katika eneo la Palestina. Katika jifunze Kiswahili hii leo tuko Tanzania kwenye Baraza la Kiswahili la Taifa BAKITA kupata ufafanuzi wa neno"KONGO"

Sauti
12'24"
Mshauri wa kike anamuonyesha mwanamke njia za kupanga uzazi katika kituo cha afya huko Sulawesi Kusini, Indonesia.
© UNICEF/Shehzad Noorani

WHO waboresha kitabu cha muongozo wa uzazi wa mpango

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO hii leo limetoa maboresho muhimu kwenye Kitabu chake cha kihistoria cha Uzazi wa mpango, ambacho kinawapa watunga sera na wafanyakazi wa sekta ya afya taarifa mpya za kuweza kufanya machaguo kuhusu dawa za uzazi wa mpango.

25 OKTOBA 2022

Hii leo kwenye Jarida la Umoja wa Mataifa tunakuletea mada kwa kina ikimulika filamu ya chapa tatu iliyotengenezwa na taasisi ya Tai Tanzania kuhusu haki za binadamu yeyote yule wakiwemo watu wenye ualbino, Mtoto Njaro ana uwezo mkubwa wa ubunifu, anakutana na changamoto kwenye jamii yake lakini hakati tamaa, anasonga mbele hadi anaibuka mshindi.

Kuna habari kwa ufupi kutoka kwake Flora Nducha akimulika:

Sauti
12'48"