03 OKTOBA 2023
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na inatupeleka Kibokoni, Kaunti ya Kilifi nchini Kenya ambako mabwawa ya samaki yamebadili kabisa maisha ya wavuvi wa eneo hilo walioathirika na mabadiliko ya tabianchi yaliyosabisha samaki kutoweka baharini na kuwakatisha tamaa ya Maisha. Lakini sasa kupitia mradi wa ufugaji samaki ulio chini ya mwamvuli wa Umoja Self-Help Group jamii hiyo ina mabwawa 17 ya samaki yanayozalisha samaki aina ya milkfish, kamba, kaa, sandfish, rabbitfish na perege au tilapia. Mshiani tanakuletea ujumbe kusu afya ya uzazi na uswa wa kijinsia.