Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

afya kwa wote

Changamoto za afya ya akili katika maeneo ya kazi
WHO

Nchi zatakiwa kufanya mageuzi kwenye sera na sheria kuhusu afya ya akili

Ikiwa leo ni siku ya Afya ya Akili duniani chini ya kauli mbiu “Afya ya akili ni haki ya binadamu wote“ Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani- WHO na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa -OHCHR wanazindua mwongozo mpya wakuzisaidia nchi kufanya mageuzi ya sheria ili kukomesha ukiukwaji wa haki za binadamu pamoja na kuongeza upatikanaji wa huduma bora za afya ya akili. 

Waziri wa Afya wa Kenya Susan Nakhumicha Wafula.
UN News

Kama COVID-19 ilivyotiliwa mkazo ifanyike hivyo kwa Kifua Kikuu

Mkutano wa ngazi ya juu kuhusu mapambano dhidi ya kifua kikuu au TB ukifanyika leo hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani, Waziri wa Afya wa Kenya Susan Nakhumicha Wafula amesema kutokomeza TB ifikapo mwaka 2030 inawezekana endapo Dunia itashikama na kuweka msokumo mkubwa kwa ugonjwa huo kama ilivyofanya wakati wa mlipuko wa janga la COVID-19.

Sauti
2'7"
WHO lazindua Baraza jipya la vijana
WHO / Chris Black

WHO lazindua Baraza jipya la vijana

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limezindua Baraza la vijana lililofanyika kuanzia tarehe 27- 30 Januari 2023 jijini Geneva Uswisi na kuwaleta pamoja viongozi vijana kutoka mashirika 22 ya vijana duniani yanayojishughulisha na masuala ya afya na masuala yasiyo ya afya.