Watoto waweka rehani maisha kuingia Ulaya, chonde chonde wasaidieni- Unicef
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesihi serikali za nchi za Ulaya kukubaliana juu ya mpango wa kikanda wa kulinda watoto wahamiaji na wakimbizi ambao wanaendelea kukumbwa na hatari kubwa na ukiukwaji mkuu wa haki za binadamu wakati wa safari za kuelekea Ulaya na ni pindi wanapowasili barani humo.