Skip to main content

Chuja:

Afrika Kusini

24 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na Mwanaisha Ulenge ni Mwanamke Mwanasayansi Mhandisi, Mbunge nchini Tanzania vilevile Mjumbe wa Shirikisho la Mabunge Duniani (IPU) na hivi karibuni akiwa katika ziara ya kikazi hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa Anold Kayanda alipata fursa ya kujadiliana naye kuhusu nafasi ya mwanamke katika sayansi na teknolojia.

Sauti
11'24"
Koketso Mukubani akisimama nje ya Kituo cha Matibabu cha Sediba Hope huko Tshwane, Afrika Kusini. Anasema wanaotumia dawa za kulevya wanapaswa kujumuishwa kwenye mipango na utekelekezaji wa kinga, tiba na huduma dhidi ya VVU na Homa ya ini C.
© UNODC

Simulizi Yangu: Kuishi na Homa ya Ini aina ya C nchini Afrika Kusini

Koketso Mokubane, mwanaume huyu raia wa Afrika Kusini alibainika kuwa na Homa ya Ini C. Amesimama nje ya kituo cha matibabu cha Sediba Hope kwenye kitongoji cha Tshwane. Koketso anafanya kazi ya kwenye ofisi ya Mtandao wa Watu wanaotumia dawa za kulevya nchini Afrika Kusini. Hili ni shirika lisilo la kiserikali linalopata msaada kupitia ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na Dawa na Uhalifu, (UNODC) kwa lengo la kutetea haki za watu wanaotumia dawa za kulevya.

03 JULAI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea kipindi maalum kuelekea siku ya kimataifa ya lugha ya Kiswahili itakayoadhimishwa wiki hii na leo tutakuwa nchini Tanzania katika Baraza la Kiswahili la taifa BAKITA. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za WHO, UNAIDS na IAEA. Mashinani tutaelekea nchini Afrika Kusini, kulikoni? 

Sauti
13'30"

23 JUNI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia umuhimu wa watumishi wa umma na walinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya kati. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Afrika Kusinin, kulikoni?

Sauti
10'41"

26 MEI 2023

Jaridani hii leo tunaangazia ripoti kuhusu matumizi ya tumbaku na wakimbizi wa Sudan. Makala tunaangazia mauaji ya kimbari nchini Rwanda na mashinani tutakupeleka nchini Chad, kulikoni?

Sauti
14'21"
Taswira ya ukumbi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
UN Photo/Manuel Elías

UNGA77 yafunga pazia, Afrika yasema sasa ni wakati wa kuwa na ujumbe wa kudumu

Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA77 umekunja jamvi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa ukiwa na maudhui: Wakati muhimu: Majawabu ya kuleta marekebisho kwa changamoto zinazofungamana. Katika siku 6 za mjadala huo nchi za Afrika zilitumia fursa kuhoji marekebisho gani yanawezekana bila kurekebisha chombo hicho ambacho kura  yenye maamuzi ya msingi inamilikiwa na wanachama 5 kati ya 193, ikiwa ni miaka 77 tangu kuudwa kwake.