Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Afrika Kusini

Mrejeshaji wa mazingira akichambua taka nchini Afrika Kusini.
Benki ya Dunia

Usajili wa warejeshaji wa mazingira Afrika Kusini waleta nuru katika kazi yao ya kuchambua taka

Sisi si wakusanya taka bali ni warejeshaji wa mazingira kwa kuepusha lundo la vitu vinavyoweza kurejelezwa kutupwa kiholela kwenye madampo. Ni kauli ya Noluthando Tutani, kutoka Chama cha Warejeshaji wa Mazingira nchini Afrika Kusini (ARO) alipozungumza kupitia video ya Benki ya Dunia kuhusu mchango wao katika kulinda mazingira.

Audio Duration
2'35"
Mnufaika wa mpango wa UN Women nchini Tanzania anatumia jiko bora lililoboreshwa ambalo limepunguza kwa kiasi kikubwa muda anaotumia kupika chakula.
© UN Women

Kulea ni jukumu la kila mtu na kunabadilisha maisha Afrika Mashariki na Kusini

Kote Afrika Mashariki na Kusini, mamilioni ya wanawake huanza siku zao mapema sana kabla hata ya jua kuchomoza. Huteka maji, huandaa chakula, kuwalea watoto na wazee, kusaidia wanajamii wenye ulemavu na kuhakikisha familia zinaendelea kama kawaida. Kazi hii ya huduma isiyolipwa ndio inayoshikilia uchumi kuendelea kuimarika lakini inakuja na gharama kubwa. Wanawake wanapata upungufu wa muda, mapato kidogo, na afya duni.

23 JULAI 2025

Hii leo jaridani tunaangazia msaada wa kibinadamu nchini Nigeria, na mradi wa nishati ya sola ya kusaidia wakulima nchini Ethiopia. Makala inakupeleka nchini Afrika Kusini na mashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.

Sauti
9'58"
UN News/Sharon Jebichii

Maoni kutoka washiriki kutoka maeneo mbalimbali waliohudhuria mkutano wa jamii za asili UNPFII

Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili, ukileta pamoja washiriki kutoka maeneo mbalimbali kote duniani. Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa walipata fursa ya kuzungumza na baadhi yao.

Sauti
3'24"

30 APRILI 2025

Hii leo jaridani tunaangazia ugonjwa wa mpox, na walinda amabini wa Umoja wa Mataifa nchini DR Congo. Makala inamuulika siku siku ya kimataifa ya muziki wa Jazz namashinani tunasalia hapa makao maku kusikia ujumbe wa mwakilishi wa shirika la watu wa jamii za Asili.

Sauti
11'14"

18 MACHI 2025

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika elimu ya mtoto wa kike kama moja ya nguzo muhimu katika jamii ukizingatia malengo endelevu ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa.Pia tunakuletea muhtasari wa habari na sauti za mashinani.

Sauti
11'24"