Ikiwa ni zaidi ya mwezi mmoja tangu kufanyika kwa mashambulizi nchini Sri Lanka yaliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 250, takribani maelfu ya wasaka hifadhi, wahamiaji na wakimbizi wengi wao kutoka Pakistan na Afghanistan, bado wamesaka hifadhi mbali na nyumba zao kwa hofu ya vipigo na manyanyaso. John Kibego na taarifa kamili.