Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

ADF

Watoto wengi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wana utapiamlo kwa vile hawapati chakula cha kutosha.
© UNICEF/Esther Ushindi

Hatua za kidiplomasia kusaidia DRC zakinzana na ukatili unaoendelea

Mikataba ya amani iliyofikiwa huko Washington nchini Marekani na Doha nchini Qatar ilileta matumaini ya hatua mpya katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Lakini wakati mawaziri wa mambo ya nje na wapatanishi wakiongeza idadi ya saini na mifumo ya ufuatiliaji, ghasia zinaendelea kumwaga damu katika maeneo ya Kivu Kaskazini na Ituri.

UN Photo/Mark Garten
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akizungumza na waandishi wa habari ( Hawapo pichani) katika Makao Makuu ya UN

Umoja wa Mataifa walaani shambulio dhidi ya shule nchini Uganda

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani vikali shambulio lililotokea jana 16 Juni 2023 dhidi ya shule ya sekondari ya Lhubirira iliyoko Mpondwe Magharibi mwa Uganda, ambalo limeripotiwa kufanywa na kundi la wanamgambo la Allied Democratic Forces (ADF).

Walnda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO wako chonjo kuhakikisha kuna usalama na hapa ni Djugu jimboni Ituru ambako walifika kuweka doria baada ya ripoti za kuweko kwa kikundi cha CODECO ambacho hushambulia raia.
MONUSCO/Force

Siku 5 za machungu kwa wakazi wa Lume, DRC: Watu 20 wauawa

Kutoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umeripoti kuwa watu wapatao 20 wakiwemo watoto wawili wameuawa wakati wa mashambulizi yaliyofanywa na wafuasi wanaodaiwa kuwa wa kikundi kilichojihami cha Allied Democrait Forces, au ADF katika siku tano zilizopita huko eneo la Lume, jimboni Kivu Kaskazini.