Kuruhusu kauli za chuki ni kushambulia moja kwa moja maadili yetu:UN
Kauli za chuki ni shambulio la moja kwa moja juu la maadili yetu ya msingi ya uvumilivu, ujumuishwaji na kuheshimu haki za binadamu. Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wakati wa uzinduzi wa mkakati na mpango wa kuchukua hatua dhidi ya kauli za chuki kwenye kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani.