Maisha ya Nelson Mandela yanatufundisha kuchagua utu – Rais wa Baraza Kuu la UN
Ili kuadhimisha siku ya kimataifa ya Nelson Mandela, Umoja wa Mataifa umefaya tukio maalum katika ukumbi wa Baraza Kuu, katika makao makuu ya umoja huo jijini New York Marekani ambapo Rais wa Baraza wa sasa, Abdulla Shahid, ameangazia maisha ya Mandela kama utafutaji usio na kuchoka wa "usawa na uhuru kwa wote".