Mchango wa Chuo Kikuu cha Mount Kenya katika kutekeleza UN SDG 9
Umoja wa Mataifa ili kuyafikia Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kama ilivyopangwa yawe yamefanikiwa kufikia mwaka 2030, waliona ni muhimu pia kuhusisha taasisi za kitaaluma duniani ndipo wakaja na kile kwa lugha ya Kiingereza walikiita ‘United Nations Academic Impact (UNAI)’, mpango unaosisitiza nafasi muhimu ya taasisi za elimu ya juu katika kuhimiza maendeleo endelevu na kuunga mkono utekelezaji wake.
Baadaye vilianzishwa vituo vya mpango huo ambavyo kila kimoja kilipewa lengo la kusongesha. Vyuo Vikuu hivyo vilivyoko katika mpango huu vimefanya Kongamano la Kimataifa kuhusu Elimu ya Juu na kimojawapo ni Chuo Kikuu cha Mount Kenya cha nchini Kenya chenye matawi mbalimbali katika Afrika Mashariki. Chuo Hiki kilichukua jukumu la kutekeleza lengo namba 9 linalolenga kuendeleza viwanda, ubunifu na miundombinu.
Profesa Peter Wanderi Mwangi ni mmoja wa washiriki wa mkutano huo amewakiwakilisha chuo hicho katika mkutano huo uliofanyika kandoni mwa Jukwaa la Kisiasa la Ngazi ya Juu kuhusu Maendeleo Endelevu (HLPF) linalohitimishwa kesho hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani. Profesa Wanderi anaeleza wanavyochangia kusongesha SDGs.