Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nimesahau yaliyopita na naganga yajayo baada ya kuuawa kwa baba yangu: Rwibutso

Mwanamume akigusa bamba la ukumbusho la kusherehekea wenzake wa Umoja wa Mataifa waliopoteza maisha wakati wa mauaji ya kimbari Rwanda 1994, chini ya bendera ya 'Kwibuka 32'.
UN News/Eugene Uwimana Emmanuel Rwibutso, kijana anayemuenzi baba yake aliyekuwa mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa ambaye aliuawa katika mauaji hayo ya kimbari.

Nimesahau yaliyopita na naganga yajayo baada ya kuuawa kwa baba yangu: Rwibutso

Amani na Usalama

Siku 100 za maombelezo ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda dhidi ya Watutsi yaliyofanyika yapata miaka 32 iliyopita zikiendelea . Leo tunakupeleka mjini Kigali nchini Rwanda kwenye Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini humo kwake Eugene Uwimana afisa habari wa ofisi hiyo ili kupata simulizi ya ya kijana anayemuenzi baba yake aliyekuwa mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa ambaye aliuawa katika mauaji hayo ya kimbari. Jina la baba huyo ni Emmanuel Turatsinze

Hilo ndilo jina la baba yake; anagusa kwenye mnara wa kumbukumbu wa wafanyakazi wa zamani wa Umoja wa Mataifa waliouawa katika Mauaji ya Kimbari dhidi ya Watutsi ya mwaka 1994. 

Mwanamume wa Rwanda mwenye ndevu amevaa kanzu nyeusi, akizungumza wakati wa mahojiano nje ya kijani kibichi nyuma.
UN News/Eugene Uwimana Emmanuel Rwibutso, kijana anayemuenzi baba yake aliyekuwa mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa ambaye aliuawa katika mauaji hayo ya kimbari.

Baba yake, Emmanuel Turatsinze, alifanya kazi katika UNDP. Mwana, Emmanuel Rwibutso, huja hapa mara kwa mara kutoa heshima zake kwa mtu ambaye hakuwahi kupata fursa ya kumwita “Baba.”

“Nilikuwa tumboni mwa mama nikiwa na umri wa miezi minne tu. Walitaka kumuua. Ilikuwa kipindi kigumu sana. Mama yangu baadaye aliniambia kwamba kutokana na mateso, wakati mmoja aliomba mtu ampige risasi. Kama hilo lingetokea, leo nisingekuwa hapa. Ninapoangalia picha hii, nahisi maumivu. Pia nahisi kuna kitu kinanisukuma mbele. Kila siku hujiuliza, je, ninahisi pengo aliloacha? Swali hilo haliniondoki kamwe, linaendelea kunisukuma mbele.”

Lakini hadithi yake haikuishia hapo hadithi yake si ya kipekee. Ni hadithi ya Rwanda. Taifa lililotekeleza usemi wa yaliyopita si ndwele na kuganga yajayo kwa kuchagua kujenga badala ya kusambaratika. 

“Mwongozo wa rais wangu, Mheshimiwa Paul Kagame, uko wazi. Ametuhamasisha kwenda haraka na kufika mbali kwa pamoja.”

Rwibutso anabeba uchaguzi huo katika jina lake katika kazi yake, na katika kila fursa ambayo kampuni yake inaunda kampuni yake, inatoa huduma za maudhui kwa njia ya video, sauti na maandishi au multimedia. 

“Hatuikimbii historia yetu ya zamani; tunapitia ndani yake kwa pamoja kuelekea jambo kubwa zaidi.”

Akiwa sasa na umri wa miaka 32, anajivunia kuunda ajira kwa vijana wengi wa Rwanda katika nchi ambako ukabila hauna nafasi, ambako fursa zinashirikiwa, na ambako anachangia katika uchumi unaokua kwa kasi.

kutoka hasara hadi urithi. Safari ya vivutio ni ukumbusho kwamba kumbukumbu si kuangalia nyuma tu, bali ni kusonga mbele kwa kusudi maalumu kwa kuchagua kukumbuka kuungana na kujenga upya Rwanda. 

Inaonyesha kwamba hata majeraha ya kina zaidi yanaweza kuzaa matumaini.