Mchango wa Tanzania katika mkutano wa 64 wa Kamisheni ya UN ya Maendeleo ya Kijamii
Malengo ya Maendeleo Endelevu
Kikao cha 64 cha Kamisheni ya Maendeleo ya Kijamii (CSocD64) kilichoanza tarehe pili mwezi huu wa Februari hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kimehitimishwa leo Februari 10.
Kamisheni hii ni chombo cha ushauri kinachohusika na nguzo ya maendeleo ya kijamii kwa maendeleo ya kimataifa.
Anold Kayanda wa Idhaa ya Umoja wa Mataifa amezungumza na mmoja wa waliohudhuria mkutano wa mwaka huu akiwakilisha Tanzania; Amon Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum na anaanza kwa kueleza zaidi kuhusu mkutano huu.