Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Muhtasari wa habari: Wajawazito; Awaza 2025; Gaza

Nyumba ya wajawazito ya kusubiri kujifungua katika mkoa wa Kunene inatoa nafasi kwa hadi wanawake 40 kukaa karibu na hospitali, pamoja na wakunga wenye ujuzi wa kutoa huduma na ushauri, pamoja na jiko la pamoja, chumba cha kula chakula na vyumba vya kula…
© UNFPA Namibia
Nyumba ya wajawazito ya kusubiri kujifungua katika mkoa wa Kunene inatoa nafasi kwa hadi wanawake 40 kukaa karibu na hospitali, pamoja na wakunga wenye ujuzi wa kutoa huduma na ushauri, pamoja na jiko la pamoja, chumba cha kula chakula na vyumba vya kulala.

Muhtasari wa habari: Wajawazito; Awaza 2025; Gaza

Afya

Ushahidi unaonesha kuwa unyanyasaji bado ni jambo la kawaida katika huduma kwa wajawazito na watoto wachanga, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, (WHO) hii leo.

Mathalani katika nchi nne, utafiti umebaini kuwa zaidi ya asilimia 40 ya wajawazito walikumbana  na kauli chafu wakati wa kujifungua ili hali zaidi ya asilimia 60 walifanyiwa uchunguzi sehemu zao za siri bila idhini yao.

Awaza

Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa nchi zisizo na bandari za baharini, LLDCs ukiendelea huko Awaza, Turkmenistan, shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP limetaka kubadilika kwa fikra ya kwamba nchi hizo kama vile Rwanda na Uganda zina mkwamo wa kibiashara na maendeleo.

Mwakilishi wa UNDP nchini Ethiopia Dkt. Samuel Doe akizindua mpango mpya wa kuonesha faida za nchi hizo kwa muunganiko wao kwa njia ya ardhi amesema…. hii leo LLDCs zinatumia vema uwepo wao kimkakati, katikati ya Afrika  na muunganiko wa kikanda kuwa vitovu muhimu vya kuunganisha nchi kiuchumi , biashara na ubunifu.

Gaza

Na wataalamu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu leo wamesema ili kuzuia vifo zaidi na mateso kutokana na njaa huko Gaza, Israel inapaswa kurejesha mara moja ruhusa kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa ya kibinadamu kuingia bila vikwazo vyovyote eneo la Palestina inalokalia kimabavu.