Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

FAO: Kilimo hifadhi na ufugaji bora wamwinua mwanamke Kigoma, Tanzania

Naam Hadija Alisido, mama wa watoto wanne na mnufaika wa mradi wa Programu ya Pamoja ya Kigoma, KJP chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO).
UN News
Naam Hadija Alisido, mama wa watoto wanne na mnufaika wa mradi wa Programu ya Pamoja ya Kigoma, KJP chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO).

FAO: Kilimo hifadhi na ufugaji bora wamwinua mwanamke Kigoma, Tanzania

Wanawake

Kutana na Hadija Alisido, mama huyu wa watoto wanne, mkulima kiongozi na mtoa chanjo ya ugonjwa wa kideri unaokumba kuku katika wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma, kaskazini-magharibi mwa Tanzania.

Hadija ni mnufaika wa mradi wa Programu ya Pamoja ya Kigoma, KJP nchini Tanania, chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) tangu mwaka 2018.

Akiishi katika eneo ambalo changamoto za kilimo ni nyingi zikichangiwa na rutuba duni ya udongo pamoja na mabadiliko ya tabia nchi, hali ya uzalishaji wa mazao ya kilimo ilionekana kuwa na matumaini kidogo mwanzoni. Lakini kupitia mafunzo ya FAO yaliyowezesha pia kupata mbegu bora na pia matumizi sahihi ya mbolea, maisha yake yalibadilika.

Naam Hadija Alisido, mama wa watoto wanne na mnufaika wa mradi wa Programu ya Pamoja ya Kigoma, KJP chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) tangu mwaka 2018.
UN News
Naam Hadija Alisido, mama wa watoto wanne na mnufaika wa mradi wa Programu ya Pamoja ya Kigoma, KJP chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) tangu mwaka 2018.

Nimeongeza mavuno

“Kwa maarifa niliyopata, nilibadilisha shamba langu la la ekari mbili, na kuongeza mavuno ya mahindi kutoka kilo 500 hadi 6,000. Kuongezeka kwa tija kuliboresha kipato changu kwa kiasi kikubwa na kuniwezesha kuwekeza katika maeneo mengine ya maisha yangu,” anasema Hadija akiwa anachambua maharage aina ya Jessica aliyovuna shambani mwake.

Hadija anasema, "nilipoanza, niliishi kwa mashaka, lakini sasa naona matunda ya juhudi zangu. Mavuno yangu ya mahindi yameongezeka, na hali ya familia yangu imeimarika. Hii ni zawadi kubwa kwa watoto wangu na kwa jamii yangu."

Eneo lao wanafuga kuku lakini kwa mazoea na hivyo kushambuliwa na magonjwa kama kideri. FAO ilimpatia Hadija mafunzo ya utoaji chanjo na sasa anatoa chanjo sio tu kwa kuku wake, bali pia wale wa jamii.

Kwa mujibu wa Hadija, juhudi zake za utoaji wa chajo zimesaidia kupunguza vifo vya kuku, kuongeza uchumi wa kijiji na kuboresha uhakika wa kupata chakula kwa familia nyingi kama litakavyo lengo namba mbili la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs la kuongeza uhakika wa kupata chakula bora.

Naam Hadija Alisido, mama wa watoto wanne akiwa na wanufaika wenzake wa mradi wa Programu ya Pamoja ya Kigoma, KJP chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) tangu mwaka 2018.
FAO Tanzania
Naam Hadija Alisido, mama wa watoto wanne akiwa na wanufaika wenzake wa mradi wa Programu ya Pamoja ya Kigoma, KJP chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) tangu mwaka 2018.

Amejenga nyumba na kununua pikipiki

Kadri shamba lake lilivyokuwa na tija, ndivyo kipato cha Hadija kilivyoongezeka. Ametumia akiba yake kujenga nyumba ya vyumba viwili, kuboresha hali ya maisha kwa familia yake.

Amenunua pia pikipiki, ambayo sio tu imerahisisha ubebabaji wa mizigo lakini pia inamsadia kuongeza kipato zaidi. Njia hii mpya ya usafiri imemuwezesha Hadija kujiingiza katika fursa zingine za kibiashara, kupanua wigo wake wa ujasiriamali.

Naweza kukidhi mahitaji ya shule ya watoto wangu

Mafanikio ya kiuchumi yamemwezesha Hadija kuwa na hakikisho la elimu kwa watoto wake. "Kwa msaada wa kilimo hiki, sasa naweza kukidhi mahitaji ya shule kwa watoto wangu. Elimu ni muhimu sana kwangu. Ninajivunia kuona watoto wangu wakikua na ndoto zao."

Nafuga pia na mbuzi

Hadija awali alifuga mbuzi wa kienyeji lakini kupitia KJP alipatiwa mbuzi wa kisasa "Nilikuwa na mbuzi wa kienyeji, lakini nilikuwa na changamoto kubwa ya kuzalisha maziwa mengi. Hata hivyo, baada ya kupokea mbuzi dume wa kisasa, hali imebadilika kabisa. Mbuzi wangu wanakuwa haraka na kunipatia maziwa  na samadi ambayo naitumia shambani,” anasema Hadija.

Mshindi wa tuzo

Safari ya mabadiliko ya Hadija haikupita bila kugundulika. Siku ya Wanawake wa Maendeleo ya Vijijini Duniani, Oktoba 15, 2023, alikabidhiwa Seti ya Vifaa vya kurahisisha shughuli za kilimo kama ishara ya kutambua mchango wake mkubwa katika kubadilisha mifumo ya chakula na kukuza usawa wa kijinsia. Ujuzi wake  katika kutumia mbinu endelevu na kuhamasisha jamii yake umeacha alama ya kudumu.

Kupitia kazi ngumu na kujitolea kwake, Hadija anaendelea kuchangia katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), kama vile "Hakuna Umaskini" (SDG 1), "Hakuna Njaa" (SDG 2), na "Maisha Kwenye Ardhi" (SDG 15).

Hadija Alisido kutoka Wilayani Kakonko mkoani Kigoma nchini Tanzania akipokea zawadi za vifaa vya kilimo wakati wa siku ya wanawake wa kijijini. Aliyevaa kofia  nyeupe ni Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Zlatan Milišić.
UN News
Hadija Alisido kutoka Wilayani Kakonko mkoani Kigoma nchini Tanzania akipokea zawadi za vifaa vya kilimo wakati wa siku ya wanawake wa kijijini. Aliyevaa kofia nyeupe ni Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Zlatan Milišić.

Ujumbe kwa wanawake

Kwa wanawake wengine Hadija ana ujumbe akisema, "Ni muhimu kujua kuwa hakuna kinachoshindikana ikiwa tutakuwa na malengo ya wazi na juhudi za kweli. Kilimo kinaweza kubadili maisha yetu, lakini lazima tuwe tayari kujifunza na kubadilika. Kila mmoja wetu ana nguvu ya kuboresha maisha yake na ya familia yake. Usikate tamaa, jifunze na tumia fursa zinazokuja mbele yako. Hakika, mabadiliko yanawezekana!"