Hatma yetu iko mikoni mwetu na muskbali wa kidijitali ni sasa: ITU
Hatma yetu iko mikoni mwetu na muskbali wa kidijitali ni sasa: ITU
Katibu Mkuu wa Muungano wa Kimataifa wa Mawasiliano ITU, Doreen Bogdan-Martin amesema, "Hatima yetu iko mikononi mwetu na mustakabali wa kidijitali ni sasa."
Ameyasema hayo katika Mkutano wa Zama Zijazo, kwenye mjdala uliobeba maudhui “Kuelekea Mustakabali wa Pamoja wa Kidijitali: Kuimarisha Ubunifu Shirikishi na Ushirikiano ili Kupunguza Mgawanyiko wa Kidijitali' yalifanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New Yorkm Marekani.
Akiwa mwenyeji wa mazungumzo hayo, Rais wa Estonia Alar Karis amesema, "Tunaamini katika manufaa ya kuunda vitu kwa Pamoja, kurejeleza na kuendeleza suluhu zilizopo tayari ili kuokoa rasilimali na kuzuia kurudiwa. Hii inapaswa kuwa kanuni yetu ya kawaida ya mwongozo, ili kuziba migawanyiko haraka.”
Pia amesema, "Mashirikika ya wadau na ushirikiano, ndani ya nchi na kimataifa, ni msingi wa jamii ya wazi ya kidigitali. Ushirikiano ni muhimu, kukusanya rasilimali na kushiriki katika kujenga uwezo, ndiyo njia ya haraka zaidi ya kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma, hasa katika nchi zinazoendelea.”
Pengo la kidijitali ni kikwazo cha maendeleo
Mwenyeji mwenza wa majadiliano hayo Mohamed Muizzu, Rais wa Jamhuri ya Maldives, amesisitiza,kwamba “Mgawanyiko huu wa kidijitali sio tu kuhusu ufikiaji wa mtandao, ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo, fursa na haki."
Doreen Bogdan -Martin, Katibu Mkuu wa ITU ameongeza kuwa "Katika ulimwengu huu, suluhu za kidijitali zinazobadilisha mwelekeo zinaweza kusongesha asilimia 70 ya malengo yote ya maedeleo endelevu, SDG. “
Lakini pia amesema kwa sasa tuna ulimwengu ambapo watu bilioni 2.6 bado hawako mtandaoni duniani kote.
Amehitimisha kwa kusema "Tunakimbizana na wakati. Hebu tulinganishe ujumuishaji wa kidijitali na kasi ya mabadiliko ya kidijitali. Wacha tusawazishe udhibiti na uvumbuzi. Na tumpe kila mtu kiti na sauti kwenye meza ya mazungumzo. Hili ni jaribu lililo mbele yetu, bado ni mtihani wetu mkuu! Hatima yetu iko mikononi mwetu na mustakabali wa kidijitali ni sasa.”